• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Muheza District Council
Muheza District Council

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Utalii
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa Kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya AFYA
    • Kilimo
    • Elimu
    • Ardhi
    • TEHAMA
      • Huduma
      • Mifumo
        • PLANREP
        • FFARS
        • PREM
        • Salary Slip Portal
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha

Bilioni 1.7 Zapatikana, Harambee ya ujenzi wa Hospitali Muheza

Posted on: March 17th, 2018

Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan awezesha upatikanaji wa Bilioni 1.7 Katika uzinduzi wa harambee ya uchangiaji wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Muheza iliyofanyika kwenye ukumbi wa Golden Tulip(Masaki) jijini Dar es Salaam Jana Machi 16, 2018.

Akizungumza na wadau walioalikwa Katika harambee Hiyo, Samia amesisitiza na kutoa wito kwa wadau na wananchi kwa ujumla Katika kuona umuhimu wa kuchangia ujenzi na uboreshwaji wa  Huduma za kijamii Kama Huduma ya Afya.

"Niwakumbushe kuwa mjenga nchi  ni mwananchi, na hivyo ujenzi huu ni hatua kubwa inayofaa kuungwa mkono na serikali, lakini pia wadau wote wa maendeleo na wanaoitakia mema Tanzania." Alisema Samia.

Aidha Samia alizitaka TAMISEMI na Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto zione namna gani zinaweza kuratibu upatikanaji wa vifaa  na watumishi wa hospitali hiyo pindi ujenzi utakapokamilika.

Pia Makamu wa Rais aliwapongeza uongozi wa Mkoa wa Tanga na Wilaya ya muheza kwa kuona changamoto na kutoa kipaombele katika upatikanaji wa huduma ya Afya Wilayani hapo, na kwa kuzingatia kuwa afya bora ni moja ya kigezo kinachochochea kwa kiasi kikubwa upatikanaji wa nguvu kazi ya taifa, na hivyo kupelekea Tanzania kufikia malengo yake ya kuwa na uchumi wa kati.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Muheza,  Mhandisi Mwanasha Tumbo alisema, katika kufanikisha ujenzi huo kila mwana Muheza ameahidi kutoa Tsh. 2000 na nguvu kazi kama mchango wao katika ujenzi wa Hospitali hiyo. 

Baadhi ya viongozi waliohudhuria hafla hiyo ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, Waziri wa TAMISEMI, Selemani Jafo, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martine Shigella na Mbunge wa Jimbo la Muheza,Mhe. Adadi Rajab.


JINSI YA KUCHANGIA UJENZI WA HOSPITALI YA WILAYA YA MUHEZA KWA KUTUMIA MITANDAO YA SIMU.

M-PESA  nenda menu *150*00#

  • Bonyeza 4:lipa kwa M-pesa
  • Bonyeza 4:Ingiza namba ya biashara
  • Ingiza 395533
  • Ingiza kumbukumbu namba (123)
  • Ingiza kiasi
  • Ingiza namba ya siri –utapokea ujumbe wa uthibitisho wa malipo

TIGO PESA  nenda menu *150*01#

  • Bonyeza 4:kulipa bili
  • Bonyeza 3:ingiza namba ya kampuni
  • Ingiza 395533
  • Ingiza kumbukumbu namba (123)
  • Ingiza kiasi
  • Ingiza namba ya siri –utapokea ujumbe wa uthibitisho wa malipo

Kwa mitandao ya ;

                AIRTEL,ZANTEL,TTCL&HALOTEL  namba ya kampuni ni 395544

Mfumo uliowezeshwa bure na kampuni ya Maxcom Africa PLC(MaxMalipo)

Tangazo

  • WANAOITWA KWENYE USAILI NAFASI ZA KAZI ZA AFYA October 12, 2024
  • MATOKEA YA NAFASI ZA UDEREVA October 10, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI VIJIJI, MADEREVA NA MWANDISHI MWENDESHA OFISI October 25, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI VIJIJI, MADEREVA NA MWANDISHI MWENDESHA OFISI October 25, 2024
  • Angalia Vyote

Habari mpya

  • RAIS SAMIA AKOSWA NA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI MAGILA AMRUHUSU AKAE KWENYE KITI CHAKE CHA RAIS

    February 28, 2025
  • RAIS SAMIA AKOSWA NA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI MAGILA AMRUHUSU AKAE KWENYE KITI CHAKE CHA RAIS

    February 28, 2025
  • RAIS SAMIA AKOSWA NA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI MAGILA AMRUHUSU AKAE KWENYE KITI CHAKE CHA RAIS

    February 28, 2025
  • MICHAEL MSECHU AONGOZA WANANCHI WA MUHEZA KUFANYA USAFI WA MAZINGIRA

    February 19, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Mhe. Samia Suluhu Hassan Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano waTanzania akizindua uchangiaji wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Muheza.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sheria Ndogo za Halmashauri
  • Ratiba ya vikao vya kisheria
  • Video za Matukio Mbalimbali
  • Huduma za Afya zinazopatikana
  • Mpango Kazi wa Halmashauri
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani na Taarifa za Kata
  • Mawasiliano ya Walimu wakuu wa Shule za Msingi na sekondari

Viunganishi linganifu

  • Ikulu
  • Mbinu mbalimbali za kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi , Milma ya Usambara Mashariki, Muheza.
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Idara kuu ya Takwimu(NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Muheza Mjini, Bomani

    Anwani ya posta: S.L.P 20 MUHEZA

    Simu: 027-2977545

    Simu ya Mkononi: 0746525653

    Barua Pepe: ded@muhezadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Muheza District Council . All rights reserved.