Mwakilishi wa Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Muheza ambaye ni Msimamizi Msaidizi ngazi ya Jimbo na Mwanasheria wa Halmashauri ya Wilaya Muheza Aisha Mhando amefungua mafunzo ya siku 2 kuanzia tarehe 23/10/2020 hadi 24/10/2020 kwa wasimamizi wasaidizi 555 wa vituo 164 vya Tarafa ya Muheza yenye kata 14 na kata ya Kwezitu.
Akizungumza katika Mafunzo hayo yaliyofanyika katika Ukumbi wa Tate plus uliopo katika kata ya Genge Bi. Aisha amewataka wasimamizi wasaidizi wa vituo hivyo wafanye kazi hiyo kwa uadilifu na utekelezaji wa yale yote watakayoelekezwa katika semina hiyo ili kuleta ufanisi mkubwa katika kazi hiyo.
Aidha amewasisitiza kutoonyesha Ushabiki wa Vyama vya siasa ili kuepukana na mgogoro unaoweza kujitokeza wakati wa zoezi la upigaji kura litakapoanza.
Sambamba na hayo, aliwaongoza wasimamizi wasaidizi hao kula kiapo cha kutunza siri kabla ya kuanza kwa mafunzo hayo.
WASIMAMIZI WASAIDIZI WA VITUO WAKIAPISHWA | WAWEZESHAJI AMBAO NI WASIMAMIZI WASAIDIZI NGAZI YA KATA WAKITOA MAFUNZO. |
|
![]() |
![]() |
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
Tangazo
Habari mpyaVideo![]() Mhe. Samia Suluhu Hassan Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano waTanzania akizindua uchangiaji wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Muheza.Video zaidiViunganishi linganifu
World visitors trackerVisitors CounterRamani ya Eneo![]() Wasiliana NasiMuheza Mjini, Bomani Anwani ya posta: S.L.P 20 MUHEZA Simu: 027-2977545 Simu ya Mkononi: 0746525653 Barua Pepe: ded@muhezadc.go.tz
Copyright ©2018 Muheza District Council . All rights reserved. |