• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Muheza District Council
Muheza District Council

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Utalii
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa Kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya AFYA
    • Kilimo
    • Elimu
    • Ardhi
    • TEHAMA
      • Huduma
      • Mifumo
        • PLANREP
        • FFARS
        • PREM
        • Salary Slip Portal
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha

Naibu Waziri OR-TAMISEMI Ampongeza Meneja TARURA-Muheza

Posted on: August 15th, 2018

Naibu Waziri Ofisi ya Raisi TAMISEMI  Mhe. Joseph George Kakunda amempongeza Mhandisi Joseph Kahoza kwa matengenezo ya barabara ya Kilomita 6 ya Mpapayu-Mgome kwa kufikia asilimia 75 ya matengenezo. 

Mhe. Kakunda ameyasema hayo katika ziara yake ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo Wilayani Muheza Agosti 15, 2018. Pia aliongeza kuwa mhandisi anafanya vizuri, hivyo basi anatakiwa kuwezeshwa ili amalize kazi yake kikamilifu kwani lengo la Serikali ni kuzipandisha hadhi barabara za mijini na vijjijini na kuwahudumia wananchi kwa ukaribu zaidi. Vilevile aliahidi kuongeza bajeti ya matengenezo ya barabara ili kuwe na barabara nyingi za changarawe na hatimaye rami.

Akisoma taarifa ya matengenezo ya barabara kwa mwaka wa fedha 2017/2018 na 2018/2019 Mhandisi Joseph Kahoza alifafanua kuwa mpaka sasa matengenezo ya barabara hiyo yamefikia asilimia 75 ambapo kiasi cha Milioni 12 (Milioni kumi na mbili) zimetumika.

Pia aliongeza kuwa katika mpango wa mwaka wa Fedha 2018/2019 kiasi cha Takribani Bilioni 1.2 (1,268,950,000) zimeidhinishwa kwa ajili ya utekelezaji wa kazi za matengenezo ya barabara za vijijini na mjini.

Aidha, Mhandisi alikumbushia maombi maalum ya barabara zilizoombewa kupandishwa hadhi kutoka barabara za Wilaya kuwa za Mkoa ambazo ni Kibaoni/Amani-Bulwa-Zirai KM 30, Kimbo-Potwe-Shambakapori km 16 na Kilulu-Mtindiro-Kwabada-Kwafungo km 40 kutokana na umuhimu wake wa kuiunganisha Wilaya ya Muheza na Wilaya za Mkinga na Korogwe.

Nae Ndugu Ismail Hassan mkazi wa Mpapayu amempongeza Mhandisi kwa matengenezo mazuri ya barabara na ameomba barabara iwekwe changarawe kwani barabara za udongo ni za msimu wa kiangazi na ikifika msimu wa mvua hazipitiki na hivyo kupelekea kushindwa kusafirisha mazao yao.

 Akiendelea kutembelea miradi mingine Mhe. Kakunda amesisitiza utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika ubora uliokusudiwa na kumalizika kwa miradi hiyo kwa wakati. Pia amesisitiza usimamizi sahihi wa fedha za miradi ya maendeleo na kuzingatia vigezo katika upatikanaji wa wakandarasi wenye uwezo.

Katika miradi iliyotembelewa, mradi wa maji Pongwe-Kitisa Muheza unatarajiwa kunufaisha watu 15,500 kwa kupata maji safi na salama kutoka asilimia 35 hadi asilimia 64, mradi wa ujenzi wa kituo cha afya Mkuzi unaotarajiwa kumalizika Septemba 15, 2018 na mradi wa ujenzi wa vyumba vinne(4) vya madarasa , mabweni mawili(2) ya wanafunzi 160 ya shule ya sekondari Muheza (Muheza High School) hatua iliyofikia mpaka sasa ni kuchimba msingi kwa kutumia nguvu za wananchi na Serikali imeahidi kutoa kiasi cha Tsh. Milioni 230 kwaajili ya kutekeleza mradi huo.


Mradi wa maji Pongwe-Kitisa Muheza




Mhe. Kakunda akisaini kitabu cha wageni katika eneo la ujenzi wa tanki la maji Kilapula

Mafundi wakiendelea na ujenzi wa tanki la maji Kilapula


Mradi wa wa ujenzi wa jengo la mama na watoto kituo cha afya Mkuzi




Mhe Kakunda akisomewa taarifa ya mradi wa ujenzi wa jengo la mama na watoto kituo cha afya Mkuzi na kaimu Mganga Mkuu Ndugu Julius Mgeni.

Mhe Kakunda akikagua ujenzi wa jengo la mama na watoto kituo cha afya Mkuzi


Mradi wa ujenzi wa majengo ya Sekondari Muheza




Naibu Waziri (wakwanza kulia) akikagua Ujenzi wa Sekondari Muheza

Naibu Waziri Kakunda akitoa maagizo ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo sekondari Muheza


Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI June 24, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI, VIBARUA WAKUSANYAJI USHURU June 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI, NAFASI ZA WATENDAJI WA VIJIJI, MADEREVA NA MWANDISHI MWENDESHA OFISI October 01, 2024
  • TANGAZO LA NYONGEZA KUITWA KWENYE USAILI October 03, 2024
  • Angalia Vyote

Habari mpya

  • RAIS SAMIA AKOSHWA NA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI MAGILA AMRUHUSU AKAE KWENYE KITI CHAKE CHA RAIS

    February 28, 2025
  • MICHAEL MSECHU AONGOZA WANANCHI WA MUHEZA KUFANYA USAFI WA MAZINGIRA

    February 19, 2025
  • WAHUDUMU WA AFYA NGAZI YA JAMII KUWAFIKIA WANANCHI VIJIJINI

    February 14, 2025
  • OMBI KUPATIWA HALMASHAURI YA PILI NDANI YA HALMASHAURI YA WILAYA YA MUHEZA

    February 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Mhe. Samia Suluhu Hassan Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano waTanzania akizindua uchangiaji wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Muheza.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sheria Ndogo za Halmashauri
  • Ratiba ya vikao vya kisheria
  • Video za Matukio Mbalimbali
  • Huduma za Afya zinazopatikana
  • Mpango Kazi wa Halmashauri
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani na Taarifa za Kata
  • Mawasiliano ya Walimu wakuu wa Shule za Msingi na sekondari

Viunganishi linganifu

  • Ikulu
  • Mbinu mbalimbali za kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi , Milma ya Usambara Mashariki, Muheza.
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Idara kuu ya Takwimu(NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Muheza Mjini, Bomani

    Anwani ya posta: S.L.P 20 MUHEZA

    Simu: 027-2977545

    Simu ya Mkononi: 0746525653

    Barua Pepe: ded@muhezadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Muheza District Council . All rights reserved.