• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Muheza District Council
Muheza District Council

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Utalii
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa Kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya AFYA
    • Kilimo
    • Elimu
    • Ardhi
    • TEHAMA
      • Huduma
      • Mifumo
        • PLANREP
        • FFARS
        • PREM
        • Salary Slip Portal
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha

Miti 600 kupandwa Muheza

Posted on: April 19th, 2018

Jumla ya miche ya miti 600 aina ya Sederea kupandwa katika shamba la Shule ya  Msingi Ngarani na Shule ya msingi Kwakifua zilizopo katika kata ya Tingeni Muheza. "Tanzania ya kijani inawezekana, panda miti kwa maendeleo ya viwanda"

Akizungumza katika Sherehe ya uzinduzi wa siku ya Upandaji Miti Wilaya ya Muheza iliyofanyika Aprili 19, 2018 katika shule hizo, Mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Muheza Mhe. Mwanasha Tumbo amesisitiza miche hiyo ipandwe katika mashamba na maeneo ya shule hizo ili pindi itakapovunwa iweze kuzisaidia shule hizo kujiendesha. Pia amewataka wataalamu wa Halmashauri kuzipatia shule hizo mbegu za zao la muhogo na mazao mengine ya muda mfupi ili kutatua changamoto ya chakula mashuleni kwa lengo la kuboresha elimu ya msingi.

Awali akisoma risala Mbele ya Mgeni rasmi, Afisa Misitu Ndugu Obadia Msemo amesema pamoja na jitihada kubwa za kuhifadhi na kupanda miti ya aina mbalimbali zinazofanyika wilayani hapo, mahitaji ya rasilimali zitokanazo na mazao ya miti ya asili kama vile Mivule, Mikingu na Minyasa na miti ya kupanda kama vile mitiki, mikaratusi, misederea na mikabela na miti mingine muhimu yameongezeka kutokana na ongezeko la viwanda na ukuaji wa soko la mazao hayo.

Ameongeza kwa kusema kuwa miti ya matunda kama vile miembe, mifenesi na minazi pia imekuwa ikishambuliwa kwa kasi kutokana na uhaba wa miti ya mbao. Ili kukabiliana na changamoto ya ongezeko hili la uhitaji tumeendelea kuwahamasisha wananchi kupanda miti ya tiki na sederea kutokana na ukuwaji wake wa haraka na thamani ya mazao yake. Pia wananchi wameendelea kuhamasishwa kupanda miti ya matunda na viungo kupitia kwa maafisa Ugani wa Halmashauri.

Wilaya ya muheza imekuwa ikipanda miti  ya matumizi mbalimbali ikiwamo ya mbao, kuni, vyanzo vya maji, vivuli na viungo kama sehemu mojawapo ya utunzaji wa mazingira. Kwa mwaka 2016/2017 jumla ya miti 2,341,181 ilipandwa na kati ya hiyo asilimia 80 (1,872,945) ya miti yote imefanikiwa kukua. kwa mwaka 2017/2018 lengo la upandaji miti kitaifa kwa kila Wilaya ni kupanda jumla ya miti 1,500,000.

Ndugu Obadia alimalizia kwa kuwasisitiza wananchi kwamba kuzilinda na kuzitunda rasilimali za misitu na mazao ni jukumu la kila mmoja wetu na  aliwakumbusha  kuwa wao ndio mlinzi namba moja wa kulinda mazingira na rasilimali zilizopo. 

Sherehe ya maadhimishi hayo pia yalihudhuliwa na Meneja wa Misitu Wilaya Ndugu Rashidi Shekivunge,  Meneja wa Misitu Msaidizi Ndugu Jaston Saria, Afisa Mazingira Ndugu Suleiman Gwaje, Afisa maendeleo ya Jamii Bi. Rose Kimaro, Muwakilishi wa Polisi(OCD), muwakilishi wa ofisi ya Takukuru Ndugu Mwezimpya na Muwakilishi wa ofisi ya Usalama.


HABARI KWA PICHA




Mkuu wa Wilaya ya Muheza (Wakatikati) akishiriki kupanda mti na mwanafunzi wa shule ya msingi Kwakifua pamoja na Meneja wa Misitu Msaidizi Ndugu Jaston Saria



Mkuu wa Wilaya ya Muheza akimkabidhi Mwalimu mkuu wa Shule ya Msingi Kwakifua Miche ya Miti ya sederea






Afisa Maendeleo ya Jamii Bi Rose kimaro akishirikiana na mwanafunzi katika zoezi la upandaji mche wa mti aina ya sederea

Wanafunzi wakiwa kandokando ya mashimo ya kupanda miti tayari kwaajili ya zoezi la upandaji miti


Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI MBALIMBALI ZA UCHAGUZI October 06, 2025
  • MAREKEBISHO YA TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO October 23, 2025
  • TANGAZO LA MAOMBI YA MPIGA KURA September 24, 2025
  • Halmashauri, Bodi ya Korosho Muheza Kugawa miche ya Korosho Bure March 07, 2018
  • Angalia Vyote

Habari mpya

  • LISHE ALAMA ZA KIJANI MUHEZA

    November 12, 2025
  • UZINDUZI WA BODI MPYA YA AFYA YA WILAYA

    November 12, 2025
  • DC SEBABILI ATOA WITO K WA WANANCHI KUTOA TAARIFA ZA WANAOTISHIA KUVUNJA AMANI SIKU YA UCHAGUZI

    October 18, 2025
  • TANZANIA KUENDELEA KUA KITOVU CHA UZALISHAJI WA KANDA YA AFRIKA MASHARIKI

    October 16, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Mhe. Samia Suluhu Hassan Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano waTanzania akizindua uchangiaji wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Muheza.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sheria Ndogo za Halmashauri
  • Ratiba ya vikao vya kisheria
  • Video za Matukio Mbalimbali
  • Huduma za Afya zinazopatikana
  • Mpango Kazi wa Halmashauri
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani na Taarifa za Kata
  • Mawasiliano ya Walimu wakuu wa Shule za Msingi na sekondari

Viunganishi linganifu

  • Ikulu
  • Mbinu mbalimbali za kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi , Milma ya Usambara Mashariki, Muheza.
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Idara kuu ya Takwimu(NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Muheza Mjini, Bomani

    Anwani ya posta: S.L.P 20 MUHEZA

    Simu: 027-2977545

    Simu ya Mkononi: 0746525653

    Barua Pepe: ded@muhezadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Muheza District Council . All rights reserved.