• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Muheza District Council
Muheza District Council

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Utalii
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa Kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya AFYA
    • Kilimo
    • Elimu
    • Ardhi
    • TEHAMA
      • Huduma
      • Mifumo
        • PLANREP
        • FFARS
        • PREM
        • Salary Slip Portal
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha

DC MUHEZA AZINDUA WIKI YA UPANDAJI MITI

Posted on: April 22nd, 2021


Mkuu wa Wilaya Muheza Mhe. Mhandisi  Mwanasha Tumbo jana tarehe 21/4/2021 amezindua wiki ya upandazi miti ambayo kwa kawaida hufanyika April 01 ya kila mwaka ikiwa lengo ni kuwahimiza wananchi kupanda miti ili kujiepusha na athari za kimazingira zinazoweza kujitokeza katika maisha ya baadae.

Akizungumza katika hafla hiyo iliyofanyika katika Shule ya Sekondari Mkurumuzi iliyopo katika Kitongoji cha Tanganyika, kata ya Tanganyika Mkuu huyo wa Wilaya amewataka wananchi wapande  miti  ili iweze kuwaongezea kipato katika kaya zao.

“Rai yangu kwenu wana muheza wenzangu kila mmoja wetu analojukumu la kupata miti na kuisimamia kikamilifu ili iweze kumletea tija katika maisha yake kwani hakuna uhai bila miti,  kupanda miti ni kutetea uhai wetu” alisema Mhe Mwanasha.

Akitoa maagizo kwa Maafisa Elimu Msingi na Sekondari wa Wilaya Muheza amewataka wahakikishe kuwa miti inapandwa katika Shule zote wilayani humo katika kipindi hiki cha Msimu wa Mvua ya Masika.

Aliendelea kuwa kila Mwananchi aliepo Wilayani humo ahakikishe anapanda miti isiyopungua mitano (5) katika kaya yake ili kumsaidia kupata kivuli na kuboresha lishe ya familia yake.

Nae Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Muheza na Mkuu wa kitengo cha Nyuki Bw. Issa Msumari amesema kupanda miti ni ustaarabu, hivyo basi wananchi wawe na desturi ya kupanda miti kwani ni mojawapo ya alama ya kukumbukwa.

“Tuwe na utamaduni wa kupanda miti itakuja kuwanufaisha wengine, tusiangalie tutavuna nini sasa hivi tuangalie mafanikio ya baadae alise Bw. Msumari.

Awali akisoma taarifa risala kwa Mgeni rasmi ambaye ni Mkuu wa wilaya Muheza Mhe. Mwanasha Tumbo Afisa Misitu Wilaya Muheza Obadia Richard Msemo amesema Wilaya Muheza ina jumla ya hekta elfu thelathini na mbili (32,000) za Misitu ya hifadhi iliyochini ya Serikali kuu  ambayo pia wananchi wa jirani hushirikishwa kurejeshea miti kwenye misitu hiyo.

Aliongeza kuwa kwa Mwaka huu  wa 2021 Wilaya ya Muheza inatarajia kupanda jumla ya Miti Milioni moja na laki tano(1,500,000) ya aina tofauti  katika maeneo mbalimbali Wilayani Muheza katika kipindi hiki cha Mvua za Masika.

Kwa upande wake Mhifadhi wa Misitu Msaidizi (TFS) wa Wilaya Muheza Jackson Saria amesema elimu na maelekezo yataendelea kutolewa kwa wananchi juu ya uvunaji endelevu wa mazao ya misitu ya kupandwa na asili ili kuhakikisha uvunaji wa mazao hayo hauleti athari za kimazingira zitakazopelekea uwepo wa jangwa.

MKUU WA WILAYA AKIZUNGUMZA MKUU WA WILAYA AKIKABIDHI MITI MKUU WA WILAYA AKIPANDA MTI MWENYEKITI HALMASHAURI AKIPANDA MTI KAIMU MKURUGENZI AKIPANDA MITI WADAU  MBALIMBALI WALIOSHIRIKI SIKU YA UZINDUZI WAKIPANDA MITI
Mkuu wa Wilaya Muheza Mhe. Mwanasha Tumbo akizungumza wakati wa kikao cha uzinduzi wa upandaji wa Miti katika Shule ya Sekondari Mkurumuzi jana tarehe 21/4/2021 Mkuu wa Wilaya Muheza Mhe. Mwanasha Tumbo(kulia) akimkabidhi Miti Diwani kata ya Tanganyika Mhe Shafii Chewaja mara baada ya kumaliza kikao cha uzinduzi wa upandaji miti jana tarehe 21/4/2020 katika shule ya sekondari Mkurumuzi. Mkuu wa Wilaya ya Muheza Mhe. Mwanasha Tumbo akipanda mti katika eneo la Shule ya Sekondari Mkurumuzi mara baada ya kikao cha uzinduzi kuisha Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza Mhe. Erasto Jerome Mhina akipanda mti katika eneo la Shule ya Sekondari Mkurumuzi iliyopo katika Kitongoji cha Tanganyika kata ya Tanganyika jana tarehe 21/4/2021. Kaimu Murugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Muheza Issa Msumari akipanda miti katika eneola Shule ya Sekondari Mkurumuzi siku ya Uzinduzi tarehe 21/4/2021.






 

Tangazo

  • WANAOITWA KWENYE USAILI NAFASI ZA KAZI ZA AFYA October 12, 2024
  • MATOKEA YA NAFASI ZA UDEREVA October 10, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI VIJIJI, MADEREVA NA MWANDISHI MWENDESHA OFISI October 25, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI VIJIJI, MADEREVA NA MWANDISHI MWENDESHA OFISI October 25, 2024
  • Angalia Vyote

Habari mpya

  • RAIS SAMIA AKOSWA NA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI MAGILA AMRUHUSU AKAE KWENYE KITI CHAKE CHA RAIS

    February 28, 2025
  • RAIS SAMIA AKOSWA NA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI MAGILA AMRUHUSU AKAE KWENYE KITI CHAKE CHA RAIS

    February 28, 2025
  • RAIS SAMIA AKOSWA NA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI MAGILA AMRUHUSU AKAE KWENYE KITI CHAKE CHA RAIS

    February 28, 2025
  • MICHAEL MSECHU AONGOZA WANANCHI WA MUHEZA KUFANYA USAFI WA MAZINGIRA

    February 19, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Mhe. Samia Suluhu Hassan Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano waTanzania akizindua uchangiaji wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Muheza.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sheria Ndogo za Halmashauri
  • Ratiba ya vikao vya kisheria
  • Video za Matukio Mbalimbali
  • Huduma za Afya zinazopatikana
  • Mpango Kazi wa Halmashauri
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani na Taarifa za Kata
  • Mawasiliano ya Walimu wakuu wa Shule za Msingi na sekondari

Viunganishi linganifu

  • Ikulu
  • Mbinu mbalimbali za kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi , Milma ya Usambara Mashariki, Muheza.
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Idara kuu ya Takwimu(NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Muheza Mjini, Bomani

    Anwani ya posta: S.L.P 20 MUHEZA

    Simu: 027-2977545

    Simu ya Mkononi: 0746525653

    Barua Pepe: ded@muhezadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Muheza District Council . All rights reserved.