• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Muheza District Council
Muheza District Council

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Utalii
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa Kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya AFYA
    • Kilimo
    • Elimu
    • Ardhi
    • TEHAMA
      • Huduma
      • Mifumo
        • PLANREP
        • FFARS
        • PREM
        • Salary Slip Portal
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha

DAS MUHEZA AFUNGUA MAFUNZO YA VIONGOZI WA MABARAZA YA KATA

Posted on: November 14th, 2020


Katibu Tawala Wilaya Muheza Bi Desderia Haule Nguza ambaye alikuwa Mgeni rasmi akimwakilisha Mkuu wa Wilaya Muheza Mwanasha Tumbo amefungua Mafunzo ya siku moja ya viongozi wa mabaraza ya kata yaliyokuwa na Washiriki 111 ambapo watendaji wa kata 37, wenyeviti wa mabaraza 37 na makatibu 37.

Hafla ya uzinduzi wa mafunzo hayo ilifanyika mnamo jana siku ya ijumaa tarehe 13/11/2020 katika ukumbi wa mikutano wa walimu (CWT).

Akizungumza katika hafla  hiyo Bi Desderia amesema lengo la mafunzo hayo ni kutoa elimu viogozi wanaosimamia kero za wananchi ili waweze waweze kuzitatua

Vilevile kuwawezesha kuwawezesha viongozi hao kutambua vyema namna ya kutenda haki ili waweze kupunguza malalamiko katika jamii.

“Niwaombe viongozi wa mabaraza ya kata Elimu mtakayoipata ikawasaidie kusikiliza kutenda haki na kutatua kero za wananchi kwani miongomi mwenu mmekuwa chanzo cha ongezeko la migogoro kwa wananchi, lakini pia natoa wito kwa wananchi waitumie wiki hii kupata elimu ya kisheria ambayo itawasaidia kufanya maamuzi mbalimbali” alisema Bi Desderia .

Aliongeza kuwa kwa kuwa hapo awali viongozi wa mabaraza hawakuwa na elimu ya ya kutosha ilipelekea baadhi yao kushindwa kuendesha kesi, Hatimaye baadhi ya viongozi walikuwa sehemu ya kuongeza migogoro katika jamii.

Kwa upande wake Muwezeshaji kutoka katika Taasisi ya Tanganyika Law Society  Ndugu Charles Livingstone Aro amezitaja sheria  3 za Mirathi kama Sheria ya Mila, Sheria ya Kiislam na Sheria ya kiserikali.

Akielezea sheria ya mirathi ya kimila Charles amesema sheria hii hutoa  mamlaka upande wa kiume kurithi mali pale itakapotokea mke au mume amefariki ambapo mali zote zitakwenda upande wa mwanaume hata kama aliefariki akiwa mke katika familia hiyo.

Wakati sheria ya kiislam humpatia mjane moja ya nane ya mali zilizoachwa na marehemu, ambapo wazazi wa marehemu hupatiwa moja ya sita ya mali na kiasi cha mali kilichobaki hupatiwa watoto wa kiume na kike.

Aliendelea kufafanua kuwa sheria ya kiserikali mgawanyo wa mali hufanyika kwa pande zote , ndugu wa marehemu, watoto wote wan je ya ndoa na walio ndani ya ndoa hugawanywa mali ya marehemu kutokana na sheria ya mtoto.

Nae  Kaimu Msajili wa Msaada wa Kisheria Wilaya Muheza Herieth Nyangasa amewataka wananchi kushiriki kikamilifu katika zoezi la siku 3 la uzinduzi wa wiki ya sheria litakalfanyika kuanzia tarehe 17/11/2020 hadi 19/11/2020 ambayo ndio siku ya kilele

Aliendelea kufafanua kuwa baada ya uzinduzi itatolewaelimu ya Mirathi na Wosia kwa wananchi watakaofika katika eneo la soko la zamani la samaki kwa siku hizo , na kuendelea kuwasisitiza wafike ili wakatatuliwe matatizo yao.

ATIBU TAWALA WILAYA MUHEZA BI DESDERIA HAULE NGUZA AKIZUNGUMZA WAKATI AKIFUNGUA MAFUNZO KATIBU TAWALA WILAYA MUHEZA BI DESDERIA HAULE(ALIEBEBA MKOBA) AKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA NA WAWEZESHAJI WA MAFUNZO( WA KWANZA KUSHOTO) NI REGIS KIVALI MWAKILISHI KUTOKA UNDP, WA PILI NI FRIDAH MWAKASYUKA KUTOKA UNDP, WA KWANZA KULIA NI CHARLES LIVINGSTONE, ALIYEVAA FLANA NI ERICK AKARO NA WA TATU KUTOKA KUSHOTO ( PICHA YA MWISHO) NI KAIMU MSAJILI MSAADA WA KISHERIA WILAYA MUHEZA HERIETH NYANGASA PICHANI NI WANASHERIA WA HALMASHAURI YA WILAYA MUHEZA, KUSHOTO NI JULIUS NGULIZI NA KULIA NI SIGSIBETH AKWILINI WAKISIKILIZA KWA MAKINI MADA ZINAZOTOLEWA KATIKA MAFUNZO YA VIONGOZI WA MABARAZA YA KATA  SEHEMU YA VIONGOZI WA MABARAZA YA KATA , WENYEVITI, MAKATIBU NA WATENDAJI WA KATA WAKISIKILIZA KWA MAKINI MAFUNZO

 

Tangazo

  • WANAOITWA KWENYE USAILI NAFASI ZA KAZI ZA AFYA October 12, 2024
  • MATOKEA YA NAFASI ZA UDEREVA October 10, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI VIJIJI, MADEREVA NA MWANDISHI MWENDESHA OFISI October 25, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI VIJIJI, MADEREVA NA MWANDISHI MWENDESHA OFISI October 25, 2024
  • Angalia Vyote

Habari mpya

  • RAIS SAMIA AKOSWA NA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI MAGILA AMRUHUSU AKAE KWENYE KITI CHAKE CHA RAIS

    February 28, 2025
  • RAIS SAMIA AKOSWA NA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI MAGILA AMRUHUSU AKAE KWENYE KITI CHAKE CHA RAIS

    February 28, 2025
  • RAIS SAMIA AKOSWA NA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI MAGILA AMRUHUSU AKAE KWENYE KITI CHAKE CHA RAIS

    February 28, 2025
  • MICHAEL MSECHU AONGOZA WANANCHI WA MUHEZA KUFANYA USAFI WA MAZINGIRA

    February 19, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Mhe. Samia Suluhu Hassan Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano waTanzania akizindua uchangiaji wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Muheza.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sheria Ndogo za Halmashauri
  • Ratiba ya vikao vya kisheria
  • Video za Matukio Mbalimbali
  • Huduma za Afya zinazopatikana
  • Mpango Kazi wa Halmashauri
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani na Taarifa za Kata
  • Mawasiliano ya Walimu wakuu wa Shule za Msingi na sekondari

Viunganishi linganifu

  • Ikulu
  • Mbinu mbalimbali za kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi , Milma ya Usambara Mashariki, Muheza.
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Idara kuu ya Takwimu(NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Muheza Mjini, Bomani

    Anwani ya posta: S.L.P 20 MUHEZA

    Simu: 027-2977545

    Simu ya Mkononi: 0746525653

    Barua Pepe: ded@muhezadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Muheza District Council . All rights reserved.