• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Muheza District Council
Muheza District Council

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Utalii
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa Kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya AFYA
    • Kilimo
    • Elimu
    • Ardhi
    • TEHAMA
      • Huduma
      • Mifumo
        • PLANREP
        • FFARS
        • PREM
        • Salary Slip Portal
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha

BENKI YA NMB YAKABIDHI BATI 200

Posted on: June 15th, 2022


Benki ya NMB imekabidhi msaada wa mabati 200 kwa Wilaya ya Muheza yenye thamani ya Shilingi Milioni nane (8,000,000) kwa ajili ya kusaidia katika ujenzi wa Shule nne za Msingi ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Serikali awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe, Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Akikabidhi msaada huo Meneja wa Benki ya NMB kanda ya Kaskazini Dismas Prosper kwa Mkuu wa Wilaya ya Muheza Halima Bulembo kwenye halfa fupi iliyofanyika katika Shule ya Msingi Kilulu alisema kuwa Taasisi hiyo ya kifedha katika Mwaka huu wa 2022 imetenga zaidi ya Bilioni mbili kwa ajili ya kutoa misaada mbalimbali hapa Nchini kote ikiwemo sekta ya Afya, Elimu ambavyo vitanufaika na vifaa kwa Mwaka huu na endapo kutaibuka majanga Benki ya NMB itasimama pamoja na wahanga katika kipindi hicho.

“Pamoja na makubwa yanayofanywa na Serikali wao kama wadau wanao wajibu wa kuunga mkono juhudi hizo za maendeleo kwa kusaidia jamii zetu ndio imefanya Benki ya NMB kuwa hapa ilipo na kubwa kuliko Benki yoyote nchini kuwa Benki ya NMB ndio Benki inayoongoza nchini huku ikiwa na Matawi 226, Mashine za ATM zaidi ya 800 nchi nzima, NMB wakala zaidi ya 10,000 na idadi ya wateja zaidi ya Milioni 4 na imefikia kote nchini kwa asilimia 100’ alisema Meneja Prosper.

Pia Meneja kanda Kaskazini Dismas Prosper alisema kuwa Benki ya NMB imetenga fedha kwa ajili ya kusomesha watoto 200 kutoka kwenye kaya duni, Wanafunzi 50 wa Vyuo vikuu na wanafunzi 150 wa kidato cha nne ambao wote watalipiwa Ada pamoja na kupatiwa mahitaji yote ya ambayo yanahitajika katika kipindi chote cha masomoyao Benki ya NMB imekuwa mtari wa mbele kuchangia huduma za kijamii kwa lengo la kurejesha sehemu ya faida yao kwa jamii.

Kwa upande wake Meneja wa NMB Wilaya ya Muheza Anna Chimalilo alisema kuwa Benki ya NMB imekabidhi msaada wa mabati 200 kwa Shule ya Msingi, Kwakibuyu  bati 50, Shule ya Msingi Mtindiro bati 50, Shule ya Msingi Kilulu bati 50 na Shule ya Msingi Bwitini bati 50, Mafanikio hayo yamekuja kufutia kupokea maombi kutoka kwa viongozi wa Wilaya ya Muheza kuomba kusaidiwa kwenye sekta mbalimbali ikiwemo ya elimu.

Awali Mkuu wa Wilaya ya Muheza  ya Mkuu wa Wilaya ya Muheza Halima Bulembo alisema kuwa anamshukuru Meneja wa Benki ya NMB tawi la Muheza Anna Chimalilo kwa kuwa bega kwa bega kwa kuisaidia Serikali kwa kila jambo linalohusu jamii kuchangia na kufika sehemu ya tukio ambapo ameomba wadau wengine kuiga mfano wa taasisi hiyoya kifedha ambayo imekuwa.

Aliongeza kuwa Waheshimiwa madiwani na walimu ambao wamenufaika na msaada huo kwenda kusimamia bati hizo ambazo wamepatiwa ili kufikia adhima ya kusaidia sekta tya Elimu

“Niwaombe Wahe. Madiwani na walimu ambao mmenufaika na msaada wa mabati kwenda kusimamia vizuri ujenzi na kuezeka mabati hayo katika madarasa huku akiahidi kutembelea kwa ajili ya kukagua ujenzi huo kama umekwenda vizuri” Mkuu wa Wilaya Bulembo alisema.

Aidha Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza Erasto Mhina alisema kuwa anaishukuru Benki hiyo kwa kitendo cha kutoa msaada wa mabati ambayo yanakwenda kuboresha elimu hivyo watakwenda kuyatumia vizuri ambapo ametumia hafla hiyo kuwasilisha maombi mawili kwa Benki ya NMB moja ni kusaidia kompyuta na Mashine ya kudurufu karatasi(photocopy)

 Mashine kwa ajili ya kutengeneza kituo cha kuchapisha Mitihani kwenye Shule zote za Muheza kwa lengo la kuinua kiwango cha elimu na ombi la pili ni kusaidia ukarabatiwa Shule ya Magila ambayo imekuwa chakavu kutokana na historia kubwa zaidi ya miaka 100 lakini Shule hiyo ina hali mbaya sana kama kuna uwezekano waangalie kwa jicho la huruma sana.




Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza Mhe Erasto Jerome Mhina akisisitiza jambo katika hafla hiyo Afisa Elimu Msingi Wilaya ya Muheza akizungumza wakati wa makabidhiano Meneja wa Benki NMB tawi la Muheza Anna Chimalilo akizungumza wakati wa hafla hiyo



Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI MBALIMBALI ZA UCHAGUZI October 06, 2025
  • MAREKEBISHO YA TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO October 23, 2025
  • TANGAZO LA MAOMBI YA MPIGA KURA September 24, 2025
  • Halmashauri, Bodi ya Korosho Muheza Kugawa miche ya Korosho Bure March 07, 2018
  • Angalia Vyote

Habari mpya

  • LISHE ALAMA ZA KIJANI MUHEZA

    November 12, 2025
  • UZINDUZI WA BODI MPYA YA AFYA YA WILAYA

    November 12, 2025
  • DC SEBABILI ATOA WITO K WA WANANCHI KUTOA TAARIFA ZA WANAOTISHIA KUVUNJA AMANI SIKU YA UCHAGUZI

    October 18, 2025
  • TANZANIA KUENDELEA KUA KITOVU CHA UZALISHAJI WA KANDA YA AFRIKA MASHARIKI

    October 16, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Mhe. Samia Suluhu Hassan Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano waTanzania akizindua uchangiaji wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Muheza.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sheria Ndogo za Halmashauri
  • Ratiba ya vikao vya kisheria
  • Video za Matukio Mbalimbali
  • Huduma za Afya zinazopatikana
  • Mpango Kazi wa Halmashauri
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani na Taarifa za Kata
  • Mawasiliano ya Walimu wakuu wa Shule za Msingi na sekondari

Viunganishi linganifu

  • Ikulu
  • Mbinu mbalimbali za kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi , Milma ya Usambara Mashariki, Muheza.
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Idara kuu ya Takwimu(NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Muheza Mjini, Bomani

    Anwani ya posta: S.L.P 20 MUHEZA

    Simu: 027-2977545

    Simu ya Mkononi: 0746525653

    Barua Pepe: ded@muhezadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Muheza District Council . All rights reserved.