• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Muheza District Council
Muheza District Council

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Utalii
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa Kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya AFYA
    • Kilimo
    • Elimu
    • Ardhi
    • TEHAMA
      • Huduma
      • Mifumo
        • PLANREP
        • FFARS
        • PREM
        • Salary Slip Portal
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha

WANANCHI WATAKIWA KUMUENZI MKAPA KWA KUWA WAWAZI NA WAKWELI

Posted on: July 29th, 2020


Wananchi wametakiwa kumuenzi aliyekuwa Rais mstaafu wa  awamu ya tatu Hayati Benjamini Wiliam Mkapa kwa kuzingatia mambo aliyoyafanya kipindi cha uhai wake yakiwemo Masuala ya Uwazi na Ukweli.

Ameyasema hayo Mkuu wa Wilaya Muheza Mhe, Mhandisi Mwanasha Tumbo wakati wa Ibada Maalum ya Maombolezo iliyofanyika jana tarehe 28/7/2020 Wilayani Muheza katika Viwanja vya Jitegemee iliyoongozwa na Mkuu huyo wa Wilaya na kuhudhuriwa na viongozi wa dini, viongozi wa vyama vya siasa, Taasisi mbalimali, watumishi wa ofisi ya Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi na Wananchi wote.

Mhe, Mkuu wa Wilaya amesema wananchi wa Wilaya hiyo walikuwa wakimuona hayati Mkapa akipita Wilayani humo akitokea uwanja wa ndege Jijini Tanga akielekea Lushoto na kwa sasa hawawezi kumuona tena hivyo waendelee kumuenzi na kumuombea.

“Ndugu zangu wana Muheza tulikuwa tunamuona Hayati Mkapa akipita hapa kwetu akitokea Uwanja wa ndege Tanga na kuelekea Wilayani Lushoto na sasa hatutamuona tena hivyo tuendelee kumuombea Mwenyezi Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi Amina” alisema Mwanasha.

“Rais Mkapa alitupikia Uji akaweka bluu bendi, na Sukari akatunywesha hivyo tumuombee kwa mola wetu amlaze mahali pema peponi Amina” alisema Mkuu wa Wilaya.

Alisema kwamba Msiba huo ni wa watu wote na Rais Magufuli, mke, watoto, na wajukuu wa Marehemu wako katika wakati Mgumu hivyo tuendeleze maombi ambayo yatakuwa faraja kwao.

Vile vile alisema kwamba wao kama Wilaya wanatoa Salamu za Pole kwa familia, ndugu, Jamaa na marafiki na kuwaombea kwa Mola azidi kuwapa faraja katika kipindi hiki kigumu.

Awali akizungumza wakati wa hafla hiyo Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya Muheza Laicky Gugu amesema Mkapa ni Kiongozi Mpiganaji aliepelekea kuanzishwa kwa Mfuko wa jamii wa TASAF, Pia alianzisha MEMKWA( ambapo lengo la Memkwa ni kutoa elimu kwa walioikosa )

Aliongeza kuwa Mkapa alikuwa Mshauri Mzuri ndani ya Chama cha Mapinduzi na hivi karibuni kabla ya kura za maoni alikuwa miongoni Mwa Wanachama waliokuwepo Dodoma ambako alitoa ushauri na mara nyiki amekuwa akijenga hoja na kuzitetea.

Nao wasanii wa Muziki Tanzania Hamisi Mwinjumaalimaarufu Mwana FA, na Mwana muziki nguli Nguza Viking alimaarufu Babu Seya wamesema kifo cha aliyekuwa rais wa awamu ya tatu Benjamini Mkapa kimewaumiza na ni pigo sana kwao kwa kuwa yeye ndie Mwanzilishi wa COSATA ambaya ni taasisi ya kusimamia haki miliki za wasanii.

MKUU WA WILAYA MUHEZA MHE, MWANASHA TUMBO AKIZUNGUMZA WAKATI WA IBADA. KATIBU TAWALA WILAYA MUHEZA AKIZUNGUMZA KABLA YA KUANZA KWA TUKIO LA IBADA VIONGOZI WA VYAMA VYA KISIASA WAKIZUNGUMZA MARA BAADA YA IBADA MAALUM YA MAOMBOLEZO SEHEMU YA WANANCHI WAKIWA KATIKA ENEO LA MAOMBOLEZO VIONGOZI WA DINI MBALIMBALI WAKIWA KATIKA HAFLA YA MAOMBOLEZO ILIYOFANYIKA UWANJANI JITEGEMEE. WANANCHI WAKIWA KWENYE FOLENI YA KUSAINI KITABU CHA MAOMBOLEZO VIONGOZI MBALIMBALI WA WILAYA MUHEZA WAKIWA KATIKA IBADA MAALUM YA MAOMBOLEZO YA RAIS MSTAAFU HAYATI BENJAMINI WILIAMU MKAPA UWANJANI JITEGEMEE. MWANAMUZIKI NGULI NGUZA VIKING ( MWENYE FLANA NYESI) AKIWA NA MKE WAKE AMBAYE NI KATIBU TAWALA WILAYA YA MUHEZA BI DESDERIA HAULE PAMOJA NA BAADHI YA WAANDISHI WA HABARI WA MKOA WA TANGA NA WA MWISHO NI MWANAMUZIKI WA BONGO FLEVA HAMISI MWINJUMA MWANA FA AKIZUNGUMZA BAADA YA IBADA.
WATU MBALIMBALI WAKISAINI KITABU CHA MAOMBOLEZO





















Tangazo

  • WANAOITWA KWENYE USAILI NAFASI ZA KAZI ZA AFYA October 12, 2024
  • MATOKEA YA NAFASI ZA UDEREVA October 10, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI VIJIJI, MADEREVA NA MWANDISHI MWENDESHA OFISI October 25, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI VIJIJI, MADEREVA NA MWANDISHI MWENDESHA OFISI October 25, 2024
  • Angalia Vyote

Habari mpya

  • RAIS SAMIA AKOSWA NA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI MAGILA AMRUHUSU AKAE KWENYE KITI CHAKE CHA RAIS

    February 28, 2025
  • RAIS SAMIA AKOSWA NA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI MAGILA AMRUHUSU AKAE KWENYE KITI CHAKE CHA RAIS

    February 28, 2025
  • RAIS SAMIA AKOSWA NA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI MAGILA AMRUHUSU AKAE KWENYE KITI CHAKE CHA RAIS

    February 28, 2025
  • MICHAEL MSECHU AONGOZA WANANCHI WA MUHEZA KUFANYA USAFI WA MAZINGIRA

    February 19, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Mhe. Samia Suluhu Hassan Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano waTanzania akizindua uchangiaji wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Muheza.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sheria Ndogo za Halmashauri
  • Ratiba ya vikao vya kisheria
  • Video za Matukio Mbalimbali
  • Huduma za Afya zinazopatikana
  • Mpango Kazi wa Halmashauri
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani na Taarifa za Kata
  • Mawasiliano ya Walimu wakuu wa Shule za Msingi na sekondari

Viunganishi linganifu

  • Ikulu
  • Mbinu mbalimbali za kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi , Milma ya Usambara Mashariki, Muheza.
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Idara kuu ya Takwimu(NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Muheza Mjini, Bomani

    Anwani ya posta: S.L.P 20 MUHEZA

    Simu: 027-2977545

    Simu ya Mkononi: 0746525653

    Barua Pepe: ded@muhezadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Muheza District Council . All rights reserved.