• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Muheza District Council
Muheza District Council

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Utalii
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa Kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya AFYA
    • Kilimo
    • Elimu
    • Ardhi
    • TEHAMA
      • Huduma
      • Mifumo
        • PLANREP
        • FFARS
        • PREM
        • Salary Slip Portal
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha

VIJANA WATAKIWA KUWA NA UTAYARI WA KUFANYA KAZI.

Posted on: February 18th, 2023


Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza Issa Suleiman Msumari amewataka vijana  kuwa na utayari na kupenda kazi zao wanazozifanya  kwani kwa kufanya hivyo kutawasaidia wao kuwa na nidhamu na kazi zao ikiwemo kujali muda, biashara  na mazingira ya kazi zao.

Ameyasema hayo alipokuwa akifunga mafunzo ya ujasiriamali kwa vijana yaliyoandaliwa na Kanisa Huru la Pentekoste nchini (FPCT). Mafunzo hayo yamefanyika  katika Ukumbi wa Ambasador uliopo wilayani Muheza Jumamosi ya Tarehe 18, February 2023.

 Ameendelea  kuwaasa wajasiriamali hao kuachana na Imani potofu za ushirikina kuamini kwamba kwenda kwa mganga kutaikuza biashara kwani hiyo ni miongoni mwa dalili zinazoonyesha kuwa uwezo wa mtu kufikiri kufika mwisho na inapelekea mtu kutopiga hatua katika biashara yake wala msingi wa biashara yake kukua na kusababisha mtu kuwa kwenye hali ile ile kila siku.


 “ Vijana wenzangu nawasihi kuwa na ujasiri na uthubutu wa kufanya mambo mbalimbali katika maeneo yenu ya kazi ikiwemo kuwa na ubunifu katika biashara zenu pamoja na kuhakikisha mnakuwa na kauli nzuri kwa wateja wenu ili kujiongezea wateja zaidi kwenye maeneo yenu ya biashara, kuwa waaminifu kwa wateja wenu hasa kwa bidhaa mnazowauzia na kutokuishi na mteja kimazoea”amesema Msumari.

Katika tukio jingine, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza amekabidhi vyeti kwa wahitimu kama kumbukumbu ya mafunzo hayo na kulishukuru Kanisa Huru la Pentekoste nchini kwa kuliomba fursa zingine za mafunzo kama haya zikitokea kuikumbuka wilaya ya Muheza na vijana wajasiriamali wa wilaya ya Muheza.

Kwa upande wake Askofu na Katibu wa jimbo la Tanga FPCT Mch. David Chema amesema lengo la mafunzo haya ni kuwajengea vijana  uwezo wa kujitegemea kiuchumi na kuwakwamua kutoka kwenye hali ngumu ya maisha. Ameendelea kwa kusema kuwa kanisa Huru la Pentekoste nchini limedumu na mradi huu kwa muda wa miaka mitatu nchi nzima likitoa elimu mbalimbali za ujasiriamali kwa vijana kama kuwafundisha jinsi ya kutengeneza bidhaa mbalimbali ikiwemo sabuni za maji,batiki na tambi zitakazowasaidia wao kuuza na kujiongezea kipato chao cha kila siku

Ameendelea  kuongeza kuwa Kanisa Huru la Pentekoste nchini limekuwa likiratibu shughuli hizi za mafunzo ya ujasiriamali kwa vijana kwa kuwalipa wawezeshaji wa semina hizo pamoja na uendeshaji wa mafunzo hayo kwa ujumla.

Mch.David Chema ameishukuru sana serikali kwa kupata kibali cha kuendesha mafunzo haya wilayani Muheza na kupata ushirikiano mkubwa kutoka kwa serikali pamoja na wadau wengine wa maendeleo.

PICHA ZA MATUKIO MBALIMBALI WAKATI WA KUFUNGA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI









Tangazo

  • WANAOITWA KWENYE USAILI NAFASI ZA KAZI ZA AFYA October 12, 2024
  • MATOKEA YA NAFASI ZA UDEREVA October 10, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI VIJIJI, MADEREVA NA MWANDISHI MWENDESHA OFISI October 25, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI VIJIJI, MADEREVA NA MWANDISHI MWENDESHA OFISI October 25, 2024
  • Angalia Vyote

Habari mpya

  • RAIS SAMIA AKOSWA NA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI MAGILA AMRUHUSU AKAE KWENYE KITI CHAKE CHA RAIS

    February 28, 2025
  • RAIS SAMIA AKOSWA NA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI MAGILA AMRUHUSU AKAE KWENYE KITI CHAKE CHA RAIS

    February 28, 2025
  • RAIS SAMIA AKOSWA NA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI MAGILA AMRUHUSU AKAE KWENYE KITI CHAKE CHA RAIS

    February 28, 2025
  • MICHAEL MSECHU AONGOZA WANANCHI WA MUHEZA KUFANYA USAFI WA MAZINGIRA

    February 19, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Mhe. Samia Suluhu Hassan Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano waTanzania akizindua uchangiaji wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Muheza.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sheria Ndogo za Halmashauri
  • Ratiba ya vikao vya kisheria
  • Video za Matukio Mbalimbali
  • Huduma za Afya zinazopatikana
  • Mpango Kazi wa Halmashauri
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani na Taarifa za Kata
  • Mawasiliano ya Walimu wakuu wa Shule za Msingi na sekondari

Viunganishi linganifu

  • Ikulu
  • Mbinu mbalimbali za kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi , Milma ya Usambara Mashariki, Muheza.
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Idara kuu ya Takwimu(NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Muheza Mjini, Bomani

    Anwani ya posta: S.L.P 20 MUHEZA

    Simu: 027-2977545

    Simu ya Mkononi: 0746525653

    Barua Pepe: ded@muhezadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Muheza District Council . All rights reserved.