• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Muheza District Council
Muheza District Council

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Utalii
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa Kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya AFYA
    • Kilimo
    • Elimu
    • Ardhi
    • TEHAMA
      • Huduma
      • Mifumo
        • PLANREP
        • FFARS
        • PREM
        • Salary Slip Portal
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha

UGONJWA WA MATENDE NA MABUSHA WATOKOMEZWA MUHEZA

Posted on: July 12th, 2020


Halmashauri ya Wilaya Muheza ina utaratibu wa kutoa huduma ya  ugawaji kinga na dawa za magonjwa yasiyopewa kipaumbele kila Mwaka lengo likiwa ni kutokmeza magonjwa ya Minyoo, kichocho,Usubi na Matende na Mabusha.

Akitoa taarifa ya maambukizi ya magonjwa yasiyopewa kipaumbele wilayani humo Mratibu wa Magonjwa yasiyopewa kipaumbele Wilaya Muheza Julius Mgeni amesema hali ya Maambukizi ya Matende na Mabusha Wilayani humo imepungua hadi kufikia chini ya asilimia mbili hili ni jambo la kujipongeza kwani ugonjwa huu ulikuwa mkubwa miaka iliyopita.

Akielezea namna ugonjwa wa matende na Mabusha unavyoenezwa Mgeni amesema  Ugonjwa huu huenezwa na Mbu ambao hupelekea kuvimba mikono, miguu, Titi na sehemu za siri

Katika hatua nyingine ameyataja magonjwa yatakayotolewa kingatiba awamu hii kuwa ni Kichocho, Minyoo na Usubi,ambapo Dawa na Kinga tiba za Magonjwa haya itatolewa kwa awamu ya kwanza na awamu ya pili ikiwa ngazi ya jamii watapatiwa kinga tiba ngazi ya jamii tarehe 6/7/2020 hadi 10/7/2020 ambapo ngazi ya Shule Ugawaji wa Dawa kinga tiba utafanyika  tarehe 26/7/2020 hadi tarehe 27/7/2020.

Aliongeza kuwa wazazi wahakikishe wanawapatia chakula cha kutosha watoto wakati wa ugawaji wa dawa na kinga tiba hizi kwani jukumu la kumuwezesha mtoto kupata chakula shuleni ni la wazazi na waachane na dhana potofu ya kuwazuia watoto wasimeze dawa hizi kwa kuzani kwamba watashindwa kupata watoto( watakuwa wagumba).

Kwa upande wake Afisa Maendeleo ya jamii Wilaya Muheza Vije Mfaume Ndwanga ametoa Wito kwa Wadau kusaidia kuchangia chakula cha watoto Shuleni kipindi cha Ugawaji wa Kinga tiba hizi

 Nae Mratibu wa magonjwa yasiyopewa kipaumbele ngazi ya Shule ambae ni Afisa Elimu vifaa Msingi Saida Mahugu amewataka viongozi wa dini kusaidia kutoa elimu kwa waumini juu ya unywaji wa dawa wiki moja kabla ya zoezi hili.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI MBALIMBALI ZA UCHAGUZI October 06, 2025
  • MAREKEBISHO YA TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO October 23, 2025
  • TANGAZO LA MAOMBI YA MPIGA KURA September 24, 2025
  • Halmashauri, Bodi ya Korosho Muheza Kugawa miche ya Korosho Bure March 07, 2018
  • Angalia Vyote

Habari mpya

  • LISHE ALAMA ZA KIJANI MUHEZA

    November 12, 2025
  • UZINDUZI WA BODI MPYA YA AFYA YA WILAYA

    November 12, 2025
  • DC SEBABILI ATOA WITO K WA WANANCHI KUTOA TAARIFA ZA WANAOTISHIA KUVUNJA AMANI SIKU YA UCHAGUZI

    October 18, 2025
  • TANZANIA KUENDELEA KUA KITOVU CHA UZALISHAJI WA KANDA YA AFRIKA MASHARIKI

    October 16, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Mhe. Samia Suluhu Hassan Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano waTanzania akizindua uchangiaji wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Muheza.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sheria Ndogo za Halmashauri
  • Ratiba ya vikao vya kisheria
  • Video za Matukio Mbalimbali
  • Huduma za Afya zinazopatikana
  • Mpango Kazi wa Halmashauri
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani na Taarifa za Kata
  • Mawasiliano ya Walimu wakuu wa Shule za Msingi na sekondari

Viunganishi linganifu

  • Ikulu
  • Mbinu mbalimbali za kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi , Milma ya Usambara Mashariki, Muheza.
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Idara kuu ya Takwimu(NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Muheza Mjini, Bomani

    Anwani ya posta: S.L.P 20 MUHEZA

    Simu: 027-2977545

    Simu ya Mkononi: 0746525653

    Barua Pepe: ded@muhezadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Muheza District Council . All rights reserved.