• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Muheza District Council
Muheza District Council

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Utalii
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa Kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya AFYA
    • Kilimo
    • Elimu
    • Ardhi
    • TEHAMA
      • Huduma
      • Mifumo
        • PLANREP
        • FFARS
        • PREM
        • Salary Slip Portal
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha

TASAF YAANZISHA UTARATIBU MPYA WA KUHAKIKI WALENGWA.

Posted on: June 17th, 2020


Mwakilishi wa Mkurugenzi wa TASAF Taifa PAULO KIJAZI amefungua kikao kazi cha wakuu wa Idara na mafunzo ya wawezeshaji wa Halmashauri ya Wilaya Muheza jana tarehe 16/6/2020 katika ukumbi wa TATE PLUS uliopo katika Kitongoji cha Genge Kata ya ili kuhakiki kaya za walengwa wa mpango wa knusuru kaya maskini na utekelezaji wa kipindi cha Pili cha Awamu ya Tatu ya TASAF.

Akisoma Hotuba ya Mkurugenzi wa TASAF Kijazi amesema tathmini ya Utekelezaji wa Kipindi cha Kwanza cha Awamu ya Tatu ya TASAF inaonyesha kuwa mpango wa kunusuru Kaya Maskini umechangia kwa kiasi kufikiwa azma ya Serikali ya kupunguza umaskini nchini. Takwimu zinaonyesha kwamba utekelezaji wa Mpango kwenye Kipindi cha Kwanza umechangia kupungua umaskini wa mahitaji ya msingi kwa kaya kwa asilimia 10 na umaskini uliokithiri umepungua kwa asilimia 12 kwa kaya maskini sana nchini.

Aliongeza kuwa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini umewezesha kaya za walengwa kujikita kwenye shughuli za kukuza kipato na kujiimarisha kiuchumi ikiwemo ufugaji, Uvuvi, 

Kilimo na biashara ndogo ndogo ambapo vijiji/mitaa/shehia zimefikiwa kwa asilimia 70.

Aliendelea kuwa Kipindi cha Pili cha Awamu ya Tatu cha Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF 111) kitatekelezwa katika Halmashauri zote 185 za  Bara na Wilaya zote za Zanzibar, utekelezaji huo utafanyika kwenye vijiji/mitaa/shehia zote nchini na kujumuisha maeneo ambayo hayakupata fursa hiyo katika Kipindi cha Kwanza cha Utekelezaji wa ambacho kimekamilika. Ikiwa Kaya Milioni moja laki nne na nusu (1,450,000) zenye zaidi ya watu Milioni 7.

Katika hatua nyingine amewataka Washiriki wa Mafunzo kuzingatia tahadhali za ugonjwa wa homa ya mapafu unaosababishwa na virus vya Corona ikiwemo kuepuka mikusanyiko isiyo ya lazima, kukaa umbali wa mita moja baina ya mtu na mtu, kuepuka kushikana mikono, kunawa Maji tiririka na sabuni na kuvaa barakoa

Aliendelea kuwa zoezi la uhakiki wa taarifa za walengwa wa Mpango wa Kunusuru kaya Maskini utafanyika kwa njia ya simu lengo ikiwa ni kuondoa taarifa za walengwa ambao hawana sifa kama vile, Viongozi, waliofariki, waliohama na wasio maskini ili kuepuka malalamiko kwa wananchi.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Muheza Nassib MMbagga amewataka wawezeshaji wazingatie mafunzo kwani atakaefanya uzembe katika kazi zoezi hilo atawajibishwa .

“Zoezi la uhakiki wa kaya za Walengwa ni jambo la Msingi na la Kitaifa na wasimamizi ni sisi , nawaombeni ambao mpo mfahamu kwamba mnatekeleza agizo la Rais Mhe John Pombe Joseph Magufuli, kiapo mtakachokula mkakifanyie kazi : mahali ambapo huelewi uliza atakaeshindwa kufuata maelekezo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake” alisema Mkurugenzi MMBAGGA.
















Tangazo

  • WANAOITWA KWENYE USAILI NAFASI ZA KAZI ZA AFYA October 12, 2024
  • MATOKEA YA NAFASI ZA UDEREVA October 10, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI VIJIJI, MADEREVA NA MWANDISHI MWENDESHA OFISI October 25, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI VIJIJI, MADEREVA NA MWANDISHI MWENDESHA OFISI October 25, 2024
  • Angalia Vyote

Habari mpya

  • RAIS SAMIA AKOSWA NA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI MAGILA AMRUHUSU AKAE KWENYE KITI CHAKE CHA RAIS

    February 28, 2025
  • RAIS SAMIA AKOSWA NA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI MAGILA AMRUHUSU AKAE KWENYE KITI CHAKE CHA RAIS

    February 28, 2025
  • RAIS SAMIA AKOSWA NA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI MAGILA AMRUHUSU AKAE KWENYE KITI CHAKE CHA RAIS

    February 28, 2025
  • MICHAEL MSECHU AONGOZA WANANCHI WA MUHEZA KUFANYA USAFI WA MAZINGIRA

    February 19, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Mhe. Samia Suluhu Hassan Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano waTanzania akizindua uchangiaji wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Muheza.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sheria Ndogo za Halmashauri
  • Ratiba ya vikao vya kisheria
  • Video za Matukio Mbalimbali
  • Huduma za Afya zinazopatikana
  • Mpango Kazi wa Halmashauri
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani na Taarifa za Kata
  • Mawasiliano ya Walimu wakuu wa Shule za Msingi na sekondari

Viunganishi linganifu

  • Ikulu
  • Mbinu mbalimbali za kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi , Milma ya Usambara Mashariki, Muheza.
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Idara kuu ya Takwimu(NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Muheza Mjini, Bomani

    Anwani ya posta: S.L.P 20 MUHEZA

    Simu: 027-2977545

    Simu ya Mkononi: 0746525653

    Barua Pepe: ded@muhezadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Muheza District Council . All rights reserved.