• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Muheza District Council
Muheza District Council

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Utalii
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa Kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya AFYA
    • Kilimo
    • Elimu
    • Ardhi
    • TEHAMA
      • Huduma
      • Mifumo
        • PLANREP
        • FFARS
        • PREM
        • Salary Slip Portal
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha

RC SHIGELA APONGEZA MUHEZA KWA KUPATA HATI SAFI

Posted on: May 21st, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Martine Shigela ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Muheza kwa kupata hati Safi kwa muda wa Miaka mitatu mfululizo kwa Mwaka 2016/2017 , 2017/2018 na 2018/2019 ambayo ni hatua nzuri ya maendeleo ya Wilaya hiyo.

Aliongeza kuwa unyenyekevu, busara na Ushirikiano baina ya Viongozi wa Halmashauri , Waheshimiwa Madiwani, na Mkuu wa Wilaya ndio nyenzo madhubuti zilizopelekea kupatikana kwa hati safi hiyo hivyo basi amewataka viongozi hao kuendelea kuchapakazi kwa weledi mkubwa ili kuleta maendeleo.

 Ameyasema hayo  tarehe 20/05/2020  katika kikao  Maalum cha baraza la Madiwani cha kuwasilisha taarifa za hesabu za Serikali (CAG) za Mwaka wa Fedha  2018/2019 kilichofanyika katika Ukumbi wa TATE PLUS  uliopo katika kata ya Genge Wilayani Muheza.

Vile vile amemuagiza Mkuu wa Wilaya Muheza Mhe, Mhandisi Mwanasha Rajabu Tumbo   kusimamia wataalam wote ambao wana pesa za Makusanyo ya Halmashauri Mkononi ambazo bado hawajaziwasilisha mahali husika warejeshe kabla ya tarehe 15/06/2020 na atakaye shindwa kurejesha ndani ya muda huu  apelekwe mahakamani.

Aidha  amewataka waheshimiwa Madiwani kutokutumia kigezo cha dini na kabila ili kujipatia nafasi katika Uchaguzi mkuu wa  mwaka 2020.

 Akitoa sababu za kutokukamilika kwa miradi miwili ya maendeleo , mradi wa maji kilapura – PONGWE- MUHEZA na Mradi wa Barabara MUHEZA- AMANI Mheshiwa Mkuu wa mkoa amesema  Ugonjwa wa homa ya mapafu unaosababishwa na virusi vya Corona umepelekea kufunga usafiri wa anga ikiwa wataalam wanaotekeleza miradi hii wanatoka Nje ya Nchi hivyo basi miradi hii itaanza hivi karibuni iwapo usafiri huo utakapofunguliwa .  

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya Muheza Mhe.Mwanasha Rajab Tumbo ameeleza kuhusuiana na kampeni kabambe ya utoaji wa elimu kwa  vitendo dhidi ya  kujikinga na Ugonjwa wa Corona inaendelea nyumba kwa nyumba ambapo wataalam mbalimbali wanahimiza juu ya uvaaji Barakoa na unawaji wa mikono na tahadhali nyingine za Corona.

Nae Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza Nassib Mmbagga ameahidi kuendelea kufuatilia na kusimamia hoja zilizobaki akiwa na lengo la kuzipunguza ili zibaki chache au kuzikamilisha kabisa.

Akizungumzia suala la  utoaji wa mikopo kwa vikundi vya wanawake,vijana na  wenye Ulemavu Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM)  Wilaya  Muheza Mhe. Mohamed Moyo ameipongeza Halmashauri na baraza la madiwani kwa kutoa mikopo hiyo kwa walengwa na kuwata kuendelea kuvipatia fedha  vikundi ili kuwakwamua kiuchumi na kuendelea kukijenga chama cha mapinduzi wilayani humo.

“pongezi Wataalam Muheza  na Madiwani kwa kutoa fedha za mikopo kwa kina mama na  wanawake wenye Ulemavu , pongezi kwa Mkurugenzi Mtendaji kwa kusimamia utoaji wa mikopo”Alisema Mohamed Moyo. 








MKUU WA MKOA WA TANGA Mhe. MARTINE SHIGELA ALIPO WASILI WILAYANI MUHEZA. MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA WILAYA MUHEZA NASSIB MMBAGGA AKIZUNGUMZA KATIKA KIKAO CHA KUWASILISHA TAARIFA YA HESABU ZA SERIKALI (CAG). PICHA YA PAMOJA BAINA YA MKUU WA MKOA Mhe.MARTINE SHIGELA NA VIONGOZI WA WILAYA YA MUHEZA BAADA YA KUHITIMISHA KIKAO. WAHESHIMIWA MADIWANI, VIONGOZI WA HALMASHAURI NA WATAALAM MBALIMBALI WAKISIKILIZA HOJA ZA KUWASILISHA TAARIFA YA HESABU ZA SERIKALI (CAG). MKUU WA MKOA WA TANGA Mhe.MARTINE SHIGELA,MKUU WA WILAYA YA MUHEZA Mhe. MWANASHA RAJAB TUMBO PAMOJA NA MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA (W) MUHEZA NASSIB MMBAGGA.
MHASIBU WA HALMASHAURI YA WILAYA MUHEZA YUSUPH AMBAKISYE JENGELA AKISOMA TAARIFA YA HOJA  YA HESABU ZA SERIKALI (CAG) 2018-2019.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Martine Shigela (wapili kushoto) akisalimiana na viongozi wa Wilaya Muheza mara baada alipo wasili wilayani humo huku akichukua tahadhali ya ugonjwa wa Corona. Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri  ya Wilaya ya Muheza Nassib Mmbagga alipokuwa akizungumza katika kikao maalum cha baraza la Madiwani wakati wakiwasilisha taarifa ya hesabu za serikali  (CAG) kilicho fanyika tarehe 20/05/2020 Muheza. Picha ya pamoja baina ya Mkuu wa Mkoa Mhe. Marine Shigela na viongozi wa Wilaya ya Muheza baada ya kuhitimisha kikao maalum cha baraza la Madiwani la kuwasilisha taarifa hesaba za Serikali kilicho fanyika tarehe 20/05/2020 Muheza. Waheshimiwa Madiwani, viongozi wa Halmashauri na Wataala mabalimbali wakiwa katika kikao maalum cha baraza la madiwani kilicho fanyika katika ukumbi wa TATE PLUS kata ya GENGE wilayani Muheza walipokuwa wakisikiliza hoja za uwasilishwaji taarifa  ya hesabu za Serikali(CAG) tarehe 20/05/2020. Mkuu wa mkoa wa Tanga Mhe. Martine Shigela(wa tatu kushoto), Mkuu wa wilaya ya Muheza Mhe. Mwanasha Tumbo (wa pili kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Muheza (wapili kulia) wa kiwa na kamati ya Urinzi na Usalama wakiwa katika picha ya pamoja baadaa ya kuhitimisha kikao maalum cha baraza cha kuwasilisha taarifa ya hesabu za serikali mwaka 2018-2019 kilicho fanyika tarehe 20/05/2020.
Mhasibu wa Halmashauri ya Wilaya Muheza Yusuph Jengela akisoma taarifa ya hoja ya uwasilishaji hesabu za serikali (CAG) ya mwaka 2018-2019 katika kikao maalum cha Madiwani kilicho fanyika tarehe 20/5/2020.

 

Tangazo

  • WANAOITWA KWENYE USAILI NAFASI ZA KAZI ZA AFYA October 12, 2024
  • MATOKEA YA NAFASI ZA UDEREVA October 10, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI VIJIJI, MADEREVA NA MWANDISHI MWENDESHA OFISI October 25, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI VIJIJI, MADEREVA NA MWANDISHI MWENDESHA OFISI October 25, 2024
  • Angalia Vyote

Habari mpya

  • RAIS SAMIA AKOSWA NA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI MAGILA AMRUHUSU AKAE KWENYE KITI CHAKE CHA RAIS

    February 28, 2025
  • RAIS SAMIA AKOSWA NA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI MAGILA AMRUHUSU AKAE KWENYE KITI CHAKE CHA RAIS

    February 28, 2025
  • RAIS SAMIA AKOSWA NA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI MAGILA AMRUHUSU AKAE KWENYE KITI CHAKE CHA RAIS

    February 28, 2025
  • MICHAEL MSECHU AONGOZA WANANCHI WA MUHEZA KUFANYA USAFI WA MAZINGIRA

    February 19, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Mhe. Samia Suluhu Hassan Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano waTanzania akizindua uchangiaji wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Muheza.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sheria Ndogo za Halmashauri
  • Ratiba ya vikao vya kisheria
  • Video za Matukio Mbalimbali
  • Huduma za Afya zinazopatikana
  • Mpango Kazi wa Halmashauri
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani na Taarifa za Kata
  • Mawasiliano ya Walimu wakuu wa Shule za Msingi na sekondari

Viunganishi linganifu

  • Ikulu
  • Mbinu mbalimbali za kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi , Milma ya Usambara Mashariki, Muheza.
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Idara kuu ya Takwimu(NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Muheza Mjini, Bomani

    Anwani ya posta: S.L.P 20 MUHEZA

    Simu: 027-2977545

    Simu ya Mkononi: 0746525653

    Barua Pepe: ded@muhezadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Muheza District Council . All rights reserved.