• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Muheza District Council
Muheza District Council

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Utalii
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa Kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya AFYA
    • Kilimo
    • Elimu
    • Ardhi
    • TEHAMA
      • Huduma
      • Mifumo
        • PLANREP
        • FFARS
        • PREM
        • Salary Slip Portal
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha

MBUNGE ADADI ATOA SHUKRANI KWA HALMASHAURI YA WILAYA MUHEZA

Posted on: June 12th, 2020

Mbunge wa jimbo la Muheza Adadi Rajab ametoa shukrani kwa viongozi na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza kwa usimamizi na utekelezaji mzuri wa ukamilishaji wa miradi ya maendeleo katika kipindi cha uongozi wake  wa miaka 5 kuanzia 2015 - 2020.

Akitoa shukrani kwa Waheshimiwa Madiwani, mkurugenzi, mtendaji, Wakuu wa Idara na Watumishi wote Adadi amesema anawashukuru kwa ushirikiano mzuri waliouonyesha kuhakikisha mabadiliko makubwa ya ongezeko la  miradi ya maji, vituo vya Afya, umeme na miundombinu ya barabara Wilayani humo ambapo hapo awali kabla ya uongozi wake havikuwepo.

Aliyasema hayo katika kikao cha baraza maalum la madiwani kilichofanyika mnamo siku ya jumanne  tarehe 9/6/2020 katika ukumbi wa Tate plus uliopo katika kitongoji cha Genge kata ya Genge Wilayani Muheza.

 akizungumzia kuhusu suala la upatikanaji wa Umeme Wilayani muheza Mhe Adadi amesema ifikapo JULY 2020 vitongoji vyote visivyokuwa na umeme vitkuwa vimepatiwa umeme.

Akielezea kuhusu Mradi mkubwa wa maji PONGWE - MUHEZA uliopo katika kata ya Mlingano Adadi amesema mpaka sasa mradi huo uko katika hatua ya mwisho ya usambazaji maji kwa wananchi ifikapo jioni ya tarehe 9/6/2020 maji yataanza kusambazwa Muheza mjini.

Aidha amewataka  waheshimiwa Madiwani kuchukua fomu za maombi ya kugombea tena nafasi zao kayika uchaguzi Mkuu wa Mwaka kwa kuwa wamefanya kazi nzuri katika kipindi chao chote walipokuwa madarakani.

"Mna kila sababu inayowafanya mrudi kwenye kata zenu ili mje mtekeleze mlichoacha, kuwa na nguvu, jiamini utarudi , wale wazee wanaostaafu tunawatakia kila la kheri, ukiona una kila sababu ya kuomba chukua fomu ukiona una wasiwasi acha kuchukua fomu,, usisubiri kutolewa kwa aibu" alisema Mhe Mbunge.

kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Muheza Nassib MMbagga ametoa taarifa ya mapokezi ya fedha kiasi cha shilingi Milioni 210 kwa ajili ya umaliziaji wa vyumba vya maabara vya Shule za Sekondari  ambapo zitapelekwa katika shule za Sekondari 7 ambazo ziko katika hatua nzuri ya umaliziaji kila shule itapewa kiasi cha shilingi Milioni 30.

Pia alitoa taarifa ya mapokezi ya gari ya wagonjwa  ( AMBULANCE) iliyotolewa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto kwa ajili ya kituo cha Afya Mkuzi ambapo ameishukuru serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na DKT JOHN POMBE MAGUFULI kwa msaada huo.

 Akijibu swali linalohusu ni lini ujenzi wa kituo cha Afya Mlesa kilichopo katika kijiji cha MLESA kata ya AMANI kitajengwa Mkurugenzi Mtendaji amesema kwa kuwa eneo la ujenzi wa kituo hicho limepatikana Mganga Mkuu Wilaya na timu yake ya wataalam wakakague eneo hilo ili ujenzi uanze haraka ambapo fedha za mapato ya ndani zitatumika kuanza ujenzi huo.

Vile vile alitoa taarifa ya kuanza kutoa huduma za Afya katika Hospitali ya Wilaya iliyopo katika kijiji cha Tanganyika Kata ya Lusanga kuwa kuanzia siku ya jumatatu tarehe 8/6/2020 huduma ya wagonjwa wa Nje ilianza kutolewa na  huduma nyingine za Maabara na huduma za Afya ya Uzazi zinatarajiwa kuanza kutolewa Mnamo Mwezi July 2020.










SEHEMU YA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA MUHEZA WAKIWA KATIKA BARAZA . MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA(W) MUHEZA NASSIB MMBAGGA AKIZUNGUMZA WAKATI WA BARAZA. MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA MUHEZA (ALIESIMAMA) MHE, BAKARI ZUBERI MHANDO AKIZUNGUMZA WAKATI WA BARAZA HILO.
WAHESHIMIWA MADIWANI WAKIWA KATIKA SALA YA PAMOJA YA KUOMBEA BARAZA KABLA YA KUANZA KIKAO MBUNGE WA JIMBO LA MUHEZA MHE, ADADI RAJAB (KUSHOTO) AKITETA JAMBO NA MHE DIWANI KATA YA NKUMBA MHE, CHARLES MHILU MARA KABLA YA KIKAO CHA BARAZA KUANZA. MWENYEKITI WA HALMASHAURI MHE, BAKARI MHANDO (KULIA) AKITETA JAMBO NA MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI NASSIB MMBAGGA KABLA YA KUANZA KWA KIKAO.




Tangazo

  • WANAOITWA KWENYE USAILI NAFASI ZA KAZI ZA AFYA October 12, 2024
  • MATOKEA YA NAFASI ZA UDEREVA October 10, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI VIJIJI, MADEREVA NA MWANDISHI MWENDESHA OFISI October 25, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI VIJIJI, MADEREVA NA MWANDISHI MWENDESHA OFISI October 25, 2024
  • Angalia Vyote

Habari mpya

  • RAIS SAMIA AKOSWA NA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI MAGILA AMRUHUSU AKAE KWENYE KITI CHAKE CHA RAIS

    February 28, 2025
  • RAIS SAMIA AKOSWA NA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI MAGILA AMRUHUSU AKAE KWENYE KITI CHAKE CHA RAIS

    February 28, 2025
  • RAIS SAMIA AKOSWA NA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI MAGILA AMRUHUSU AKAE KWENYE KITI CHAKE CHA RAIS

    February 28, 2025
  • MICHAEL MSECHU AONGOZA WANANCHI WA MUHEZA KUFANYA USAFI WA MAZINGIRA

    February 19, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Mhe. Samia Suluhu Hassan Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano waTanzania akizindua uchangiaji wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Muheza.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sheria Ndogo za Halmashauri
  • Ratiba ya vikao vya kisheria
  • Video za Matukio Mbalimbali
  • Huduma za Afya zinazopatikana
  • Mpango Kazi wa Halmashauri
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani na Taarifa za Kata
  • Mawasiliano ya Walimu wakuu wa Shule za Msingi na sekondari

Viunganishi linganifu

  • Ikulu
  • Mbinu mbalimbali za kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi , Milma ya Usambara Mashariki, Muheza.
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Idara kuu ya Takwimu(NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Muheza Mjini, Bomani

    Anwani ya posta: S.L.P 20 MUHEZA

    Simu: 027-2977545

    Simu ya Mkononi: 0746525653

    Barua Pepe: ded@muhezadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Muheza District Council . All rights reserved.