• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Muheza District Council
Muheza District Council

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Utalii
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa Kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya AFYA
    • Kilimo
    • Elimu
    • Ardhi
    • TEHAMA
      • Huduma
      • Mifumo
        • PLANREP
        • FFARS
        • PREM
        • Salary Slip Portal
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha

DIWO YATOA MAFUNZO KWA WAJASIRIAMALI MUHEZA

Posted on: March 5th, 2022


Taasisi ya Dira ya wanawake inayojishughulisha na uchakataji wa matunda, mbogamboga, utunzaji bustani na usafi wa majumbani (DIWO) imetoa mafunzo kwa wajasiriamali wilayani Muheza tarehe 3/3/2022 katika ukumbi wa CWT kwa ajili ya kuwasaidia vijana kibiashara na kujiingizia kipato.

Akizindua Mafunzo hayo, Mkurugenzi wa DIWO Bi Shamsa Danga, amesema lengo la Ziara yake ni kuhamasisha vijana wa kata ya Kicheba pamoja na wanafunzi wa Sekondari ya Kicheba 150 wenye umri kuanzia miaka 16-24 kujiunga kwenye Taasisi ili kuweza kupatiwa Mafunzo ya Ujasiriamali.

Aliendelea kuwa, Mradi huu ni wa mwaka mmoja na utafanyika kwa awamu tatu,ambapo, Awamu ya kwanza ni usindikaji wa matunda na mbogamboga, awamu ya pili ni utunzaji wa bustani na ikiwa awamu ya tatu ni usafi wa majumbani. Mafunzo haya yanahusisha ujuzi wa ufungashaji na kuongeza thamani ya bidhaa zilizochaguliwa kama vile; tomato sauce, chilli sauce, pactin, jam ya fenesi, juisi ya fenesi, viungo, matunda yaliyokaushwa, pickles, jam ya matunda, crips na pipi za maganda ya machungwa.  

“Mradi huu utatekelezwa katika Kata ya Kicheba Wilayani Muheza kwasababu ya uwepo wa  eneo pamoja na  matunda ya aina mbalimbali, mbogamboga pamoja na viungo”. Alisema Bi Shamsa Danga.

Nae Diwani wa Kata ya Kicheba Mhe. Hamisi Mhina Mkodingo alipata nafasi ya kuzungumzia uwepo wa maeneo mbalimbali katika Kata ya Kicheba na kuahidi kutoa ushirikiano katika taasisi hiyo juu ya upatikanaji wa maeneo pamoja na malighafi zitakazotumika katika Mradi huo zitapatikana kwa wakati.

Pia Diwani wa Kibaha wa viti maalum Mhe Lidya amemshukuru Mkurugenzi wa DIWO Bi Shamsa Danga kwa jitihada za kuleta Mradi huu utakaohusisha ujenzi wa kiwanda na kuelezea kuwa ni kuunga mkono jitihada za Mhe Rais Samia Hassani Suluhu katika kazi kubwa anayoifanya. Lakini pia amethibitisha uwepo wa vifaa na jitihada zilizofanyika katika usajili wa mwanzo wa kiwanda hicho huko SIDO kinachotarajiwa kujengwa katika kata ya kicheba.

Aidha, kwa upande waVijana walioshiriki kwenye uzinduzi wa mradi huo walijitokeza na kuelezea namna walivyopokea mafunzo hayo na kuwa utawasaidia kuongeza ujuzi na kipato cha kaya.

Afisa Kilimo, Silvester Mzirai ameelezea namna ya upatikanaji wa matunda na viungo katika Wilaya ya Muheza na kuelezea changamoto mbalimbali namna matunda yanavyoharibika na kwa namna gani Mradi huu na upatikanaji wa kiwanda utapunguza changamoto hiyo.

Kijana Joyce Fadhili ambaye pia ni Mjumbe wa DIWO alitoa maelezo ya Mradi huo na ni kwa namna gani amekuwa Mjasiriamali wa kuweza kutengeneza sabuni na mafuta kwa kutumia mimea asilia kama vile parachichi na kuelezea kuwa bidhaa hizo ni nzuri na zinafaa kwa matumizi ya ngozi bila kuleta madhara ya aina yoyote.

Mwisho Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza Bw. Amiri Msuya ambaye pia ni mhamasishaji wa vijana katika Wilaya ya Muheza,ametoa shukurani na kuelezea kuwa Mradi huu umekuja katika wakati sahihi kwasababu imeenda sambamba na Miradi mingine kama Bomba la Mafuta na kuelezea kuwa itasaidia kuleta chachu ya mafanikio ya mtu mmoja mmoja na kwa Serikali kwa ujumla kwasababu itainua kipato cha wananchi kwa kutoa ajira pamoja na serikali kupitia kodi za Wananchi.

Kwa kumalizia amesema wadau wote wanakaribishwa kuwekeza na kupatiwa vibali pamoja na kupatiwa msaada wowote ambao uko ndani ya uwezo wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza.



Mkurugenzi wa taasisi ya DIWO (wa kwanza kulia) akiwa katika picha ya pamoja na diwani kata ya kicheba (wa pili kulia ) Mhe. Hamisi Mkodingo,diwani wa  viti maalum  Kibaha (mwenye kilemba cheusi)  Mhe. Lidya Mgaya na vijana walioshiriki kwenye uzinduzi uliofanyika siku ya alhamisi tarehe 3/3/2022 katika ukumbi wa CWT- MUHEZA.
Kaimu Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Muheza ambaye pia ni mhamasishaji vjana Wilaya Muheza Amiri Msuya akizungumza katika Uzinduzi wa mafunzo ya Vijana wajasiriamali.



Tangazo

  • WANAOITWA KWENYE USAILI NAFASI ZA KAZI ZA AFYA October 12, 2024
  • MATOKEA YA NAFASI ZA UDEREVA October 10, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI VIJIJI, MADEREVA NA MWANDISHI MWENDESHA OFISI October 25, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI VIJIJI, MADEREVA NA MWANDISHI MWENDESHA OFISI October 25, 2024
  • Angalia Vyote

Habari mpya

  • RAIS SAMIA AKOSWA NA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI MAGILA AMRUHUSU AKAE KWENYE KITI CHAKE CHA RAIS

    February 28, 2025
  • RAIS SAMIA AKOSWA NA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI MAGILA AMRUHUSU AKAE KWENYE KITI CHAKE CHA RAIS

    February 28, 2025
  • RAIS SAMIA AKOSWA NA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI MAGILA AMRUHUSU AKAE KWENYE KITI CHAKE CHA RAIS

    February 28, 2025
  • MICHAEL MSECHU AONGOZA WANANCHI WA MUHEZA KUFANYA USAFI WA MAZINGIRA

    February 19, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Mhe. Samia Suluhu Hassan Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano waTanzania akizindua uchangiaji wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Muheza.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sheria Ndogo za Halmashauri
  • Ratiba ya vikao vya kisheria
  • Video za Matukio Mbalimbali
  • Huduma za Afya zinazopatikana
  • Mpango Kazi wa Halmashauri
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani na Taarifa za Kata
  • Mawasiliano ya Walimu wakuu wa Shule za Msingi na sekondari

Viunganishi linganifu

  • Ikulu
  • Mbinu mbalimbali za kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi , Milma ya Usambara Mashariki, Muheza.
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Idara kuu ya Takwimu(NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Muheza Mjini, Bomani

    Anwani ya posta: S.L.P 20 MUHEZA

    Simu: 027-2977545

    Simu ya Mkononi: 0746525653

    Barua Pepe: ded@muhezadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Muheza District Council . All rights reserved.