• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Muheza District Council
Muheza District Council

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Utalii
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa Kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya AFYA
    • Kilimo
    • Elimu
    • Ardhi
    • TEHAMA
      • Huduma
      • Mifumo
        • PLANREP
        • FFARS
        • PREM
        • Salary Slip Portal
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha

BARAZA LA MADIWANI MUHEZA LAWATAKA WANANCHI WOTE KUVAA BARAKOA.

Posted on: May 1st, 2020

Kikao cha baraza la Madiwani kilichofanyika April 30, 2020 katika ukumbi wa TATE PLUS uliopo katika kata ya Genge kimeazimia Wananchi wote wanapotoka majumbani na wanapokuwa katika maeneo yao ya kazi wavae barakoa ikiwa ni tahadhari ya ugonjwa wa  Corona.

Akizungumza katika kikao hicho Mwenyekiti wa Halmashauri ambae ni Mwenyekiti wa kikao cha baraza la Madiwani na Diwani kata ya Ngomeni Mhe, Bakari Zuberi Mhando amesema kwa kuwa hali ya Maambukizi inaongezeka kila siku hapa nchini ni vyema kila Mwananchi anapotoka nje ya nyumba yake avae barakoa ili kujikinga na ugonjwa wa homa ya mapafu unaosababishwa na virusi vya Corona.

Pia alimtaka Mmiliki wa Vyombo vya Muziki SADICK mwenye tabia ya kupiga Muziki usiku maeneo ya njia ya kwenda Magila aache tabia hiyo mara moja kwani itasababisha mkusanyiko na kupelekea kuleta Maambukizi Wilayani.

Nae Mkuu wa Wilaya Muheza Mhe Mhandisi Mwanasha Rajab Tumbo amewataka wanachi kuacha tabia ya Mkusanyiko msibani wanaotakiwa kuhudhuria kwenye tukio hilo ni watu wasiozidi kumi (10) tu ili kuepuka msongamano katika eneo husika.

Pia aliwataka Waheshimiwa Madiwani wakatoe elimu katika maeneo yao kwani suala la ugonjwa wa Corona linahitaji elimu ya kutosha kwa wananchi, pia aliwataka watoe msaada wa michango ya vifaa tiba au fedha ili kuweza kufanikisha kutokomeza janga hili.

“Twendeni Waheshimiwa tukatoe elimu kwa wananchi wetu , tunao wajibu sisi kama viongozi kutekeleza jukumu hili” alisema Mkuu wa Wilaya Muheza.

Akijibu swali aliloulizwa ni kwa namna gani Halmashauri inasaidia katika kupambana na Ugonjwa huu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Muheza Nassib MMbagga amesema Halmashauri inasaidia kununua vifaa tiba na kinga kwa ajili ya wataalam waliopo katika vituo vya kutolea huduma za Afya.

Akieleze kuhusu kuwachukulia hatua za kisheria wale wote watakaokuwa wameshindwa kuvaa barakoa na kuchukua tahadhari nyingine juu ya ugonjwa wa Corona Mkurugenzi Mtendaji Wilaya amesema kwa atakaeshindwa kuweka Ndoo ya Maji na Sabuni nyumbani na katika eneo la biashara yake baada ya elimu inayotolewa na wataalam huko majumbani faini itakuwa ni TZS 50,000/ (Elfu hamsini) pia amelitaka baraza kuweka sheria ya pamoja ya kusimamia agizo hili.

“Tuacheni tuendelee kutoa elimu kwa wananchi, wale wajeuri watakaoshindwa kutekeleza maelekezo tutahangaika nao, nitachukua hatua, nikiwachukulia hatua mnyamaze” alisema Mkurugenzi MMBAGGA.

Akifafanua namna ya uvaaji wa barakoa Mganga Mkuu Wilaya amesema Barakoa moja huvaliwa kila baada ya Masaa 4-6 hivyo basi kila mmoja anatakiwa kutembea na barakoa zaidi ya mbili mfukoni mwake, aliongeza kuwa mtu anapovaa barakoa hatakiwi kujishikashika usoni kwani anaweza kujisababishia maambukizi.

Aidha alijibu swali la ushonaji wa barakoa za vitambaa kuwa barakoa ya kitambaa inatakiwa kuwa na’ layer’ tatu ambapo layer ya katikati inatakiwa kuwa na stiff ili kusaidia hewa kupita kwa urahisi na material ya kitambaa kinachotakiwa ni Cotton.

Aliongeza kuwa barakoa ya kitambaa ikivuliwa ihifadhiwe vizuri kwenye mfuko ukifika nyumbani ifuliwe kwa sabuni nyingi na kunyooshwa kabla haijavaliwa tena wakati barakoa za madukani (disposable) zikivuliwa zichomwe moto.

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Muheza Nassib Mmbagga akisisitiza Uvaaji wa barakoa wakati wa kikao cha baraza la Madiwani kilichofanyika April 30, 2020 katika ukumbi wa Tate Plus.  Diwani kata ya Genge Mhe,  Mtiga  Adam Lubawa akizungumza wakati wa Kikao cha baraza la Madiwani kilichofanyika April 30, 2020 katika Ukumbi wa Tate Plus 


Mkuu wa Wilaya Muheza Mhe,  Mhandisi Mwanasha Rajab Tumbo (aliye simama) akizungumza wakati wa baraza la Madiwani April 30, 2020 katika Ukumbi wa Tate Plus uliopo Kata ya Genge Diwani Kata ya Misalai Mhe,  David Bughe akizungumza wakati wa baraza tarehe 30/4/2020 katika Ukumbi wa Tate plus
SEHEMU YA WAJUMBE WA BARAZA 

BAADHI YA WATAALAM WAKIZUNGUMZA WAKATI WA BARAZA
 

DMO Flora kessy.      Meneja TARURA                                         kahoza 



Tangazo

  • WANAOITWA KWENYE USAILI NAFASI ZA KAZI ZA AFYA October 12, 2024
  • MATOKEA YA NAFASI ZA UDEREVA October 10, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI VIJIJI, MADEREVA NA MWANDISHI MWENDESHA OFISI October 25, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI VIJIJI, MADEREVA NA MWANDISHI MWENDESHA OFISI October 25, 2024
  • Angalia Vyote

Habari mpya

  • RAIS SAMIA AKOSWA NA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI MAGILA AMRUHUSU AKAE KWENYE KITI CHAKE CHA RAIS

    February 28, 2025
  • RAIS SAMIA AKOSWA NA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI MAGILA AMRUHUSU AKAE KWENYE KITI CHAKE CHA RAIS

    February 28, 2025
  • RAIS SAMIA AKOSWA NA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI MAGILA AMRUHUSU AKAE KWENYE KITI CHAKE CHA RAIS

    February 28, 2025
  • MICHAEL MSECHU AONGOZA WANANCHI WA MUHEZA KUFANYA USAFI WA MAZINGIRA

    February 19, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Mhe. Samia Suluhu Hassan Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano waTanzania akizindua uchangiaji wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Muheza.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sheria Ndogo za Halmashauri
  • Ratiba ya vikao vya kisheria
  • Video za Matukio Mbalimbali
  • Huduma za Afya zinazopatikana
  • Mpango Kazi wa Halmashauri
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani na Taarifa za Kata
  • Mawasiliano ya Walimu wakuu wa Shule za Msingi na sekondari

Viunganishi linganifu

  • Ikulu
  • Mbinu mbalimbali za kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi , Milma ya Usambara Mashariki, Muheza.
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Idara kuu ya Takwimu(NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Muheza Mjini, Bomani

    Anwani ya posta: S.L.P 20 MUHEZA

    Simu: 027-2977545

    Simu ya Mkononi: 0746525653

    Barua Pepe: ded@muhezadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Muheza District Council . All rights reserved.