• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Muheza District Council
Muheza District Council

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi na Manunuzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Utalii
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa Kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya AFYA
    • Kilimo
    • Elimu
    • Ardhi
    • TEHAMA
      • Huduma
      • Mifumo
        • PLANREP
        • FFARS
        • PREM
        • Salary Slip Portal
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
      • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha

WAZAZI WATAKIWA KUTENGA MUDA KUZUNGUMZA NA WATOTO WAO

Posted on: March 9th, 2020


Mkuu wa Wilaya Muheza Mhe Mwanasha Rajab Tumbo amewataka wazazi kutenga muda kuongea na watoto wa ili waweze kufahamu mambo mbalimbali wanayokumbana nao pindi wawapo Shuleni na Mitaani.

Akizungumza katika Sherehe za Maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani iliyofanyika jana tarehe 8/3/2020 katika uwanja wa Jitegemee Mhe Mwanasha amesema watoto wamekuwa wakifanyiwa vitendo vya ukatili kama ubakaji , ulawiti hivyo basi wazazi wawe imara kusimamia watoto wao ili kuhakikisha wanasoma vyema na kuweza kuisaidia nchi hapo baadae.

”tuwasikilze watoto wetu wawe wa kike au kiume kwani mara nyingi wamekuwa wakibakwa na kulawitiwa mara kwa mara wanapokuwa shuleni na majumbani na wengine hufanyiwa vitendo hivi na ndugu zetu , watoto wenzao na waume zetu, wageni wanaokuja majumbani mwetu tuhakikishe tunawasimamia vyema ili waweze kufikia malengo yao ya kuhudumia  Nchi hii ya Tanzania” alisema Mhe Tumbo.

 Sambamba na hayo  amewataka wanawake kupendana na kusaidiana pindi wa patapo matatizo badala ya kuleteana maneno ya fitna, Majungu  na uongo ili kuleta tija na maendeleo katika taifa kwani wao ndio chanzo kikubwa cha kuinua uchumi wa Taifa

“Ndugu zangu nataka niwaaminishe kuwa uchumi wa nchi hii unaongozwa na wanawake , hivyo basi tupendane, na kusiadiana pale unapoona mwenzako ana nafasi fulani usipeleke maneno ya fitna wala majungu, anapokosea mwenzako msahihishe na msaidie. alisema Mkuu wa Wilaya Muheza.

Aliongeza kuwa wanawake wajiunge katika vikundi vya ujasiriamali ili waweze kupatiwa mikopo na waweze kuongeza kipato cha kaya kwani Halmashuri ikupitia mapato yake ya ndani hutenga 10% kila mwaka kwa ajili ya kukopesha vijana asilimia 4, wanawake asilimia 4 wanawake na wenye ulemavu asilimia 2 hivyo wanawake wachangamkie fursa hii na wahakikishe wanarejesha kwa wakati.

Vile vile amewataka wanawake wanapopata matatizo wapeleke migogoro yao kwenye vyombo vya kisheria kama vile kwenye madawati ya jinsia yaliyopo polisi ambako haki na usawa wa mwanamke huzungumziwa .

Kwa upande mwingine ameitaka jamii kuepukana na tabia ya kushikana mikono pindi wasalimianapo, kukumbatiana, kubusiana na kuwataka wanawe mikono mara kwa mara ikiwa ni tahadhari dhidi ya Ugonjwa wa korona ambao mpaka sasa umeua watu wengi Nchini China.

Awali akisoma Risala kwa mgeni rasmi ambaye ni Mkuu wa Wilaya Muheza Mhe, Mwanasha Rajabu ,  Diwani viti maalum  kata ya Amani Mhe Mariamu Nyota amesema tafiti zinaonyesha kuwa wanawake wanafanya kazi nyingi kwa saa 16 hadi 18 kwa siku ikiwa na maana kwamba wana saa 6 hadi 8 tu za kulala, kupumzika na kushiriki shughuli nyingine hali inayosababishwa na mila na desturi zilizojengeka katika jamii hali hii husababisha wanawake kubebeshwa mzigo mzito wa majukumu hali inayowafanya wakose muda wa kujiendeleza.

Aliongeza kuwa baadhi ya mila na desturi potofu huvunja haki za mwanamke kama tabia za ukeketaji wa watoto wa kike kuwanyima wanawake haki ya kurithi mali ya marehemu mume wake, kuwanyima haki ya kupata elimu, kuwaozesha katika umri mdogo, kuwanyima haki ya kumiliki ardhi ni baadhi ya mifano michache ya ukiukwaji mkubwa wa haki za wanawake kwa kisingizio cha Mila na Desturi.

Aliendelea kuwa baadhi ya wanawake hufanyiwa vitendo vya ukatili wa kimwili au kingono na wenza wao na hivyo kuathiri maendeleo yao ya kiafya, kisaikolojia na kiuchumi.

Akiitaja kauli mbiu ya mwaka huu inayosema “Usawa kwa Maendeleo ya Tanzania ya sasa na baadaye”  ameishukuru Serikali kwa jitihada zake za kujenga usawa wa kijinsia kwa wanawake na wanaume kwa kuwawezesha kupata mikopokutoka Halmashauri yenye asilimia sawa na wanaume pia kwa kuanzisha majukwaa yanayolenga kusimamia usawa wa wanawake na wanaume 

Aidha siku ya wanawake duniani iliadhimishwa kwa kuandamana toka bomani mpaka Uwanja wa Jitegemee,  upimaji wa HIV, ushauri nasaha, ukaguaji wa mabanda ya wajasiriamali, mashindano ya kukimbiza kuku, kuvuta kamba na  kucheza mpira wa miguu baina ya wanawake wa Tarafa ya Muheza na Tarafa ya Amani sanjari na hafla ya usiku wa Mwanamke uliofanyika katika ukumbi wa TARECU ambako maonyesho ya Mavazi ya tamaduni mbali mbali yalionyeshwa.

WANAWAKE WAKIWA KWENYE MAANDAMANO MHE, DIWANI VITI MAALUM KATA YA AMANI MARIAM NYOTA AKISOMA RISALA KWA MGENI RASMI


Tangazo

  • WANAOITWA KWENYE USAILI NAFASI ZA KAZI ZA AFYA October 12, 2024
  • MATOKEA YA NAFASI ZA UDEREVA October 10, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI VIJIJI, MADEREVA NA MWANDISHI MWENDESHA OFISI October 25, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI WATENDAJI VIJIJI, MADEREVA NA MWANDISHI MWENDESHA OFISI October 25, 2024
  • Angalia Vyote

Habari mpya

  • RAIS SAMIA AKOSWA NA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI MAGILA AMRUHUSU AKAE KWENYE KITI CHAKE CHA RAIS

    February 28, 2025
  • RAIS SAMIA AKOSWA NA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI MAGILA AMRUHUSU AKAE KWENYE KITI CHAKE CHA RAIS

    February 28, 2025
  • RAIS SAMIA AKOSWA NA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI MAGILA AMRUHUSU AKAE KWENYE KITI CHAKE CHA RAIS

    February 28, 2025
  • MICHAEL MSECHU AONGOZA WANANCHI WA MUHEZA KUFANYA USAFI WA MAZINGIRA

    February 19, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Mhe. Samia Suluhu Hassan Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano waTanzania akizindua uchangiaji wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Muheza.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Sheria Ndogo za Halmashauri
  • Ratiba ya vikao vya kisheria
  • Video za Matukio Mbalimbali
  • Huduma za Afya zinazopatikana
  • Mpango Kazi wa Halmashauri
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani na Taarifa za Kata
  • Mawasiliano ya Walimu wakuu wa Shule za Msingi na sekondari

Viunganishi linganifu

  • Ikulu
  • Mbinu mbalimbali za kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi , Milma ya Usambara Mashariki, Muheza.
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Idara kuu ya Takwimu(NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Muheza Mjini, Bomani

    Anwani ya posta: S.L.P 20 MUHEZA

    Simu: 027-2977545

    Simu ya Mkononi: 0746525653

    Barua Pepe: ded@muhezadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Muheza District Council . All rights reserved.