Majukumu ya Idara ya Mipango na Ufuatiliaji ni kama ifuatavyo:-
1. Kusimamia Uandaaji wa mpango wa utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi kila mwaka.
2. Kuratibu ufanisi wa mifuko ya Halmashauri: LGCDG, Mfuko wa Jimbo na fedha za mapato ya ndani.
3. Uratibu na utayarishaji wa Mipango shirikishi katika Kata zote za Halmashauri kupitia Mfumo wa O&OD.
4. Uratibu na utayarishaji wa Mpango na Bajeti ya kila mwaka ya Halmashauri.
5. Kusimamia uandaaji wa mipango kazi (Action Plans) ya bajeti za kila mwaka na kuziwasilisha katika ngazi husika..
6. Kuratibu uandaaji wa maandiko ya miradi mbalimbali ya maendeleo.
7. Kuratibu maandalizi na utekelezaji wa Mpango wa Matokeo Makubwa sasa (BRN)
8. Kuratibu maandalizi ya Sera na Mpango Mkakati wa Halmashauri
9. Kuratibu uandaaji wa taarifa mbalimbali za Halmashauri pamoja na taarifa za utekelezaji wa maagizo kutoka mamlaka za juu za serikali
Muheza Mjini, Bomani
Anwani ya posta: S.L.P 20 MUHEZA
Simu: 027-2977545
Simu ya Mkononi: 0746525653
Barua Pepe: ded@muhezadc.go.tz
Copyright ©2018 Muheza District Council . All rights reserved.